Nyenzo-rejea ya 1: VVU na UKIMWI katika Afrika

Nyenzo-rejea ya Mwalimu ya kutumia katika kupanga au kurekebisha pamoja na wanafunzi

TOLEO LA WAVUTI:

http://www.avert.org [Tip: hold Ctrl and click a link to open it in a new tab. (Hide tip)]

Huu ni ukurasa wa maskani wa wavuti wa shirika linaloitwa AVERT – Shirika la Kimataifa la kusaidia watu wenye VVU na UKIMWI lililoko Uingereza, lenye lengo la kuzuia VVU na UKIMWI duniani.

Utapata taarifa muhimu kwa walimu katika sehemu hii.

TOLEO LA MAKALA:

  • A.Ukweli pamoja na takwimu muhimu zinazohusu VVU na UKIMWI kwa nchi za Afrika zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara

    Sehemu ya AVERT inatoa takwimu ambazo wanafunzi wako wanaweza kuuliza maswali juu yake. Pia ina mwongozo muhimu wa kuelewa takwimu.

    Hapa pana muhtasari wa takwimu kwa ajili ya Afrika. Utapata undani zaidi kuhusiana na nchi yako kwenye sehemu ya Wavuti hii.

    Afrika sehemu ya kusini mwa Jangwa la Sahara imeathiriwa sana na VVU na UKIMWI kuliko ukanda wo wote ule duniani. Mwishoni mwa mwaka 2005, ilikadiriwa kuwa watu milioni 24.5 walikuwa wanaishi na VVU na kiasi cha milioni 2.7 yalikuwa ni maambukizo mapya yalitokea katika mwaka huo. Katika mwaka uliopita tu mlipuko huo ulikatisha maisha ya watu wanaokadiriwa kuwa milioni 2 katika ukanda huu. Zaidi ya watoto milioni 12 ni yatima wa UKIMWI.

    Mama na mtoto katika hospitali ya Wilaya ya Nsanje, Malawi, wote wana VVU+.

    Ni sasa tu ambapo kiasi cha mlipuko kimeweza kuwa bayana katika nchi nyingi za Kiafrika, kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu wenye VVU wanaougua. Bila kufanya jitihada za kuzuia, kutibu na kuwatunza watu dhidi ya VVU/UKIMWI, inatarajiwa kuwa idadi ya vifo vinavyotokana na UKIMWI itaendelea kupanda. Hii inamaanisha kuwa athari za mlipuko katika jamii hizi zitaonekana zaidi katika kipindi cha miaka kumi au zaidi ijayo. Madhara yake kijamii na kiuchumi tayari yameshaonekana, siyo tu katika sekta ya afya lakini pia katika elimu, viwanda, kilimo, usafiri, rasilimali watu na uchumi kwa ujumla.

    Nchi mbalimbali za Afrika zimeathirikaje?

    Kiwango cha kuenea kwa VVU kinatofautiana sana baina ya nchi za Afrika. Katika nchi za Somalia na Senegali kiwango cha kuenea ni chini ya asilimia moja (1%) cha idadi ya watu wazima, ambapo Afrika Kusini na Zambia ni kati ya asilimia 15-20% ya watu wazima ambao wameathirika.

    Katika nchi nne za kusini mwa Afrika, kiwango cha kuenea kwa VVU kwa watu wazima kitaifa kimepanda juu kuliko ilivyokuwa imefikiriwa na sasa kinazidi asilimia 20%. Nchi hizi ni Botswana (24.1%), Lesotho (23.2%), swaziland (33.4%) na Zimbabwe (20.1%).

    Afrika Magharibi ilikuwa haijaathirika sana na VVU, lakini viwango vya kuenea kwa VVU vinaongezeka. Kuenea kwa VVU kunakadiriwa kuzidi asilimia 5% katika nchi ya Kameruni (5.4%), Kodivaa (7.16) na Gaboni (7.9%).

    Mpaka hivi karibuni, kiwango cha kuenea kwa VVU na UKIMWI kilikuwa kiko chini katika nchi ya Nijeria, nchi ambayo ina watu wengi kuliko nchi zote za Afrika zilizoko kusini mwa Jangwa la Sahara. Kiwango kilipanda taratibu kutoka chini ya asilimia 2% katika mwaka 1993 hadi asilimia 3.9% katika mwaka 2005. Lakini baadhi ya miji ya Nijeria tayari imeshakuwa na kiwango cha maambukizo ambacho ni kikubwa sawa na vile vilivyoko katika nchi ya Kameruni. Tayari kiasi cha Wanijeria milioni 2.9 wanakadiriwa kuwa wanaishi na VVU.

    Imechukuliwa kutoka: AVERTing AIDS and HIV, Website

  • B.Ukweli na takwimu muhimu kuhusiana na VVU na UKIMWI kwa Tanzania

    36, 766,356: Makisio ya idadi ya watu, Julai 2005.

    1,400,000: makisio ya watu waliokuwa wanaoishi na VVU/UKIMWI mwishoni mwa 2005.

    Makisio ya Asilimia 6.5% ya watu wazima (umri 15-49) waliokuwa wanaoishi na VVU/UKIMWI mwishoni mwa mwaka 2005.

    710,000: makisio ya idadi ya wanawake (umri 15-49) wanaoishi na VVU/UKIMWI mwishoni mwa 2005.

    110,000: Makisio idadi ya watoto (umri 0-14) wanaoishi na VVU/UKIMWI mwishoni mwa 2005.

    140,000: Makisio ya idadi ya vifo vilivyotokana na UKIMWI kwa mwaka 2005.

    1, 000,000: makisio ya idadi ya watoto waliopoteza mama au baba au wazazi wote wawili kwa UKIMWI na walikuwa hai na chini ya umri wa miaka 17 mwishoni mwa mwaka 2005.

    Vyanzo: Ripoti ya UNAIDS ya mwaka 2006 kuhusu Mlipuko wa UKIMWI Duniani -Mei 2006 (UNAIDS 2006 Report on the Global AIDS Epidemic – May 2006);; Kitabu cha CIA cha Kweli Duniani 2005 (CIA World Factbook 2005).

Nyenzo-rejea ya 2: Hali ya darasa