Somo la 3

‘Kuakisi’ ni kutafakari juu ya kile kilichotokea na kuona jinsi ya kufanya vizuri zaidi wakati mwingine. Baada ya kuwa umejaribu shughuli mpya, inasaidia sana kuakisi/kutafakari juu ya mafanikio na kitu gani kinahitaji maboresho. Fanya mchakato wa ‘Panga-Tenda-Rekodi-Tafakari’ kuwa sehemu ya mazoea yako ya kila siku (angalia Nyenzo Rejea 1 ).

Sasa una mkusanyiko mzuri wa michezo, unaweza kuitumia michezo hii kama msingi wa shughuli za ujifunzaji, na kama msingi wa kuakisi/kutafakari na uboreshaji. (kazi hii pia inaweza kufanywa kwa kutumia hadithi.)

Nyenzo Rejea 3: Michezo ya maneno ina michezo kadhaa ambayo unaweza kuijaribu pamoja na wanafunzi wako.

Uchunguzi kifani ya 3: Vitenzi vya Kiswahili katika wimbo wa kurukaruka maneno

Bi Alison aliimba wimbo wa kurukaruka maneno wakati alipokuwa mtoto pale Mazimbu, Morogoro. Aliamua kuutumia wimbo huo kufundishia wanafunzi wake wa darasa la 2 maneno kadhaa na virai vya wakati uliopo vya Kiswahili.

Kwanza wanafunzi waliuimba kwa Kiswahili na kisha aliwasaidia kuuimba kwa Kiingereza.

Alimpatia kila mwanafunzi kipande cha karatasi chenye kitenzi (m.f. la, nywa, cheka, kohoa, ruka, kimbia, rukaruka) kilichoandikwa kwenye karatasi hiyo. Alihakikisha kuwa kila mtoto anafahamu maana ya neno hilo na jinsi ya kufanya vitendo vinavohusiana na neno hilo.

Alimwambia kila mwanafunzi mmoja mmoja afanye vitendo bila maneno, na darasa liliimba ubeti mpya: ‘Antoni, msichana huyu anafanya nini? Antoni, msichana anacheka,’ n.k.

Baada ya somo, alitafakari kuhusu:

Kile kilichokwenda vema;

Kile ambacho hakikwenda vema sana;

Kile kilichomshangaza;

Kile ambacho angekibadili kama angerudia lile somo.

Bi Alison alishangazwa na jinsi wanafunzi walivyoutumia muda katika kujifunza toleo la Kiswahili lakini pia jinsi wanafunzi waliufurahia muda. Aliona kuwa alihitaji kutumia muda zaidi katika shughuli hii, na pia kufundisha maneno machache zaidi.

Wiki iliyofuata, alitumia toleo la aina nyingine la Kiswahili lililokuwa na wimbo wa kurukaruka maneno kwa jinsi ile ile, ya kutunga beti zenye aina mbalimbali za vyakula.

(Angalia Nyenzo Rejea 4: Wimbo wa kurukaruka maneno kutoka katika wimbo wa kurukaruka maneno wa Igbo.)

Shughuli muhimu: Kujifunza kutokana na mkarara, wimbo au mchezo

Je, kuna mkarara kwenye makusanyo ya darasa lako ambao lugha yake inaweza kubadilishwa na kuwa kama lugha ya nyongeza na kuweza kutumiwa katika kuhamasisha ujifunzaji wa lugha?

Bainisha sentensi katika mkarara ambayo neno (au maneno) yangeweza kubadilishana nafasi kwa zamu. Kwa mfano, ‘Anacheka’ lingeweza kubadilishana nafasi na (Anaruka, anarukaruka, anakimbia’ n.k.). Kila mwanafunzi, au kikundi, kinaweza baadaye kuimba ubeti mpya, wenye neno jipya katika sentensi ya mwanzo.

Ingeweza hata kufurahisha zaidi kama maneno au sentensi yataweza kuambatana na vitendo.

Panga jinsi utakavyopanga darasa lako kwa ajili ya kuimba/ kukariri na kuigiza (zoezi hili ni mbadala’. (Huu ni mfululizo wa sentensi, ambazo zinafanana isipokuwa kwa neno au kishazi kimoja. Sentensi hizi zinatumika kufanya mazoezi ya mitindo ya lugha.)

Kama hutafanikiwa, utatakiwa kujaribu wimbo mwingine, au njia nyingine ya kuendesha shughuli hii.

Nyenzo-rejea ya 1: Duara la tenda - tafakari