Somo la 3

Mawasiliano sio kuhusu maneno tu. Siku hizi magazeti mengi yana picha nyingi kuliko zamani na vitabu vya siku hizi vina vielelezo vingi zaidi kuliko vitabu vya zamani. Watoa matangazo hutumia picha katika mabango, katika majarida na katika televisheni (luninga) ili kuuza bidhaa zao. Skrini za kompyuta huchanganya maneno na picha katika hali ya kusisimua. Wanafunzi wanahitaji kuandika na kusoma matini ambazo zinachanganya maelezo ya mazungumzo (maneno) na michoro (picha). Ukiwa mwalimu majukumu yako ni:

Kuwa na habari za sasa za mambo yanayowafurahisha wanafunzi;

Ukijumlisha na shughuli za michoro ya ubunifu (kwa mfano, ubunifu wa michoro ya vifurushi vya kuchukulia bidhaa za madukani, mabango ya matangazo, matangazo ya biashara) katika lugha na masomo ya kusoma na kuandika.

Sehemu hii inazingatia uchoraji wa gamba la vitabu vya watoto vinavyohusu hadithi, mashairi, nyimbo na michezo.

Uchunguzi kifani ya 3: Kujadili na kutengeneza magamba ya vitabu

Mwalimu Malaitji anawahimiza wanafunzi wake wa somo la Kiingereza wa darasa la 6 kuuliza maswali wakati wa somo lao la kusoma kuhusu maneno na misemo ambayo wanaisikia au kuisoma lakini hawaielewi. Siku moja asubuhi, mwanafunzi aliliambia darasa kuwa amesikia mhusika mmoja wa mchezo wa kuigiza katika televisheni akimwambia mwenzie kuwa ‘Usihukumu kitabu kwa kuangalia gamba lake.’ Mwalimu Malaitji aliwauliza wanafunzi wake mawazo kuhusu msemo huo una maana gani na kwa nini ulitumika katika mchezo huo wa kuigiza. Baada ya muda mfupi wa majadiliano, wanafunzi walielewa kuwa uchoraji wa gamba la kitabu unaweza au usiweze kutoa wazo zuri kuhusu yaliyomo katika kitabu. Kwa mtazamo huo, mtu aonekanavyo au asemavyo inaweza isiwe kielelezo cha jinsi mtu huyo alivyo ‘ndani mwake’.

Mwalimu Malaitji aliamua kuendeleza majadiliano. Aliwataka wanafunzi darasani kufikiri kuhusu shabaha za gamba la vitabu, halafu waangalie gamba la kitabu cha hadithi ambacho alileta darasani. Wanaweza kueleza kuhusu hadithi inahusu nini kwa kuangalia gamba la kitabu? Wamependa nini au ni kitu gani ambacho hawakukipenda kuhusu gamba hilo la kitabu? Gamba hilo linaweza kuboreshwa, na kama jibu ni ndiyo, linaweza kuboreshwaje? Baada ya mjadala hai na kusoma hadithi kwa wanafunzi, aliwataka wafanye kazi katika vikundi vya wanafunzi wanewane kutengeneza gamba jipya kwa ajili ya kitabu hiki na aliwapa makaratasi ya kufanyia kazi. Walipomaliza, mwanafunzi mmoja kutoka kila kikundi alitoa maelezo darasani kwa nini wamechora gamba la kitabu katika namna waliyochagua. Mwalimu Malaitji aliyabandika magamba ya vitabu katika ukuta wa darasa.

Shughuli muhimu: Kuandika vitabu na kutayarisha gamba la vitabu

Baada ya kumaliza kuandika na kuchora kwa ajili ya vitabu vya hadithi, wanafunzi sasa wako tayari kutayarisha gamba la kitabu. Unaweza kutumia migongo ya mabango, karatasi za maboksi na vifaa vingine ‘vilivyotupwa’, hasa kama vifaa havitoshi shuleni kwenu. Tazama Nyenzo-rejea muhimu: Kuwa mwalimu mwenye msaada katika hali zenye changamoto kwa mawazo zaidi.

Waoneshe watoto magamba ya vitabu na waulize sifa nzuri za gamba hilo (Tazama Nyenzo-rejea: Sifa za matayarisho ya gamba la vitabu).

Watake kila kikundi kutayarisha gamba la kitabu chao. Wanapaswa kukubali kuhusu maneno watakayotumia, michoro na sehemu watakapoiweka na kuamua waamue nani ataandika au kuchora kila sehemu ya gamba.

Zungukia vikundi kujadiliana matayarisho yao na wasaidie na kuwaongoza wanapotengeneza gamba lao la kitabu

Vipe muda vikundi kukamilisha vitabu vyao.

Mtake mwanafunzi mmoja wa kila kikundi kuonesha kitabu chao na wahimize wanafunzi wengine katika vikundi kukisoma.

Viweke vitabu katika maktaba ya darasa.

Unafikiri wanafunzi wako wamejifunza nini katika shughuli hii?

Je, vitabu hivyo vilisomwa na wanafunzi wengine vilipowekwa katika maktaba ya darasa?

Kwa watoto wadogo, soma hadithi au mashairi na watake wachore picha kwa ajili ya gamba la kitabu au ndani ya kitabu.

Nyenzo-rejea 1: Jinsi hadithi zinavyoandikwa kuwa vitabu