Somo la 2

Kwa kila kazi yoyote ya hisabati au swali ulilotayarisha kwa ajili ya wanafunzi wako, kuna nduni za msingi –nduni ambazo zinafasili jinsi kazi ilivyo, na mbinu zinazoweza kusaidia kulifanya swali hilo.

Karibu maswali yote yana nduni hizi za msingi, zinazoshikiliwa na seti fulani ya nduni za juujuu. Kama mwalimu, lazima uwasaidie wanafunzi wako waelewe kwamba wanapogundua tu nduni za juujuu, kule kuzibadili hakuleti athari yoyote kuhusu jinsi ya kulifanya swali hili. Mbinu za kufanyia swali zinabaki zilezile. (Tazama Nyenzo-rejea 2: Njia za kuwasaidia wanafunzi kufanya maswali .)

Uchunguzi kifani ya 2: Kiini cha swali

Shumi aliliandika swali hili ubaoni:

Katika familia moja, kuna watoto wawili: Adam ana miaka 8 na Antoni ana miaka 4. Nini wastani wa umri wa watoto hawa? Baadhi ya wanafunzi walitaka kujibu haraka, lakini, kabla ya kupata jibu, aliwataka waangalie vizuri lile swali –lilikuwa ni swali la aina gani. Je, kulikuwa na kitu chochote ambacho angeweza kukibadili bila kuathiri jibu?

Baadhi ya wanafunzi waligundua kuwa wangeweza kubadili majina ya wanafunzi bila kubadili jibu. Shumi aliwapongeza.

Alitoa hesabu rahisi ya kujumlisha ubaoni (1+1=2) na kisha alisema,

‘kama nikibadili namba hapa,’ (Kuandika 2+5=7) ‘jibu si lile lile, bali ni

aina ile ile ya jibu. Kuhusu swali letu la wastani, tunaweza kubadili nini, bado tukaendelea kuwa na jibu la aina ileile?’

Baadhi ya wanafunzi walipendekeza kuwa wangeweza kubadili umri wa wanafunzi pamoja na majina. Kisha Shumi aliuliza, ‘Je,lingekuwa ni jibu lile lile kama tungesema ng’ombe badala ya watoto?’

Waliendelea kuongea namna hii, mpaka walipong’amua kuwa wangeweza kubadili kitu walichokifikiria, namba na nduni za vitu hivi vya kuhesabia, bila kubadili jibu linalotafutwa.Kisha wanafunzi walianza kuandika na kujibu kwa kutumia mifano mingi ya majibu ambayo hawakuyatarajia.

Shughuli ya 2: Kipi kinaweza kubadilika, kipi lazima kibaki kama kilivyo?

Kwanza jaribu shughuli hii mwenyewe. Andika maswali haya ubaoni kwako:

Bwana Ogunlade anatengeneza ukuta wa matofali ya sementi

upande mmoja wa eneo lake ili kuwazuia mbuzi. Alitengeneza ukuta wenye kimo cha matofali 10 na urefu wa chini wa matofali

20. Jumla atahitaji matofali mangapi? Liambie darasa lako lifanye swali hili. Kagua jibu lao.

Kisha, waambie wanafunzi katika vikundi vya wanafunzi wanewane au watanowatano wajadili jibu hilo kwa pamoja na kitu gani kinaweza kubadilishwa katika swali na bado kiini cha swali kikabaki kama kilivyo na swali likafanywa kwa njia ileile.

Viambie vikundi vitoe mfano mwingine, wenye kiini cha swali kama hicho, ilimradi kazi ya msingi isibadilike.

Vikundi vibadilishane swali na kikundi kingine na vitafute jibu.

Je, wanafunzi wanatakiwa kufanya swali hili jipya kwa njia ile ile?