Somo la 1

Namba Ruwaza za Kimstatili

1. X

2. X

3. X

4. 2x2

5. X

6. 2x3, 3x2

7. X

Hii inafaa kwa namba za mstatili. Unatarajia hapo pawe na namba chache au nyingi za ‘mstatili’ kuliko ‘namba mraba’ , na unaweza kueleza kwa nini? Kuangalia namba zinazounda maumbo ya mstatili ni njia moja ya wanafunzi ya kutalii hesabu za kuzidisha (au kugawanya) kwa njia ya kuona na kufanya, na vile vile kufanya hesabu za jumla kwa kichwa na kwa kuandika.

Kujaribu kufanya uchunguzi mwenyewe ili kuona ni wapi wanafunzi wanaweza kupata shida na kupanga jinsi ya kuwasaidia wale wanaojitahidi kutakusaidia wewe ili ufanikiwe zaidi katika kuwasaidia wanafunzi katika ujifunzaji.

Uchunguzi kifani ya 2: Kucheza mchezo wa kutafuta zao mtiririko

Bibi Ali alipanga kuwauliza wanafunzi wake watafute namba mbalimbali za mstatili kwa kutumia kanuni za kuzidisha.

Aliamua kuwa na mashindano ya darasa. Aliligawa darasa katika timu mbili na kuiambia kila timu ichague mfungaji goli. Mchezo ulikuwa kwamba anaandika namba ubaoni na mwanafunzi wa kwanza aliyetoa namba/vipengele viwili ambavyo ni sahihi kwa namba hiyo aliweza kuipatia timu yake pointi/alama. Bibi Ali alieleza kwamba kungekuwa na majibu zaidi ya moja - wakati mwingine majibu mengi. Baadaye alionesha mfano darasani kwa kuandika 6 na kusema kwamba angempa mtu yeyote alama ambaye angesema ‘2 mara 3’ au ‘3 mara 2’ au ‘1 mara 6’ au ‘6 mara 1’. Darasa lilifurahia mchezo na lilisisimka sana. Bibi Ali alifurahi sana, kwani alikuwa ameshapanga kwamba mchezo huu ungewasaidia wanafunzi wake katika shughuli zao nyingine. 

Katika kazi zilizofuata baadaye, mara nyingi alicheza mchezo huu na wanafunzi alipokuwa amebakiwa na dakika tano za kumaliza somo kwa siku hiyo.

Shughuli ya 2: Kuzidisha kwa kutumia vihesabio

Utahitaji vihesabio 20, vizibo vya chupa, maharage au mawe kwa kila kikundi cha wanafunzi wanne au watano.

Anza kwa kuligawa darasa katika vikundi vyao na kuwapatia vihesabio.

Nakili au chora ubaoni jedwali lililopo katika Nyenzo Rejea 2: Jedwali la kuzidisha ili wanafunzi walinakili kwa ajili ya kuandikia majibu yao.

Viambie vikundi vichukue vihesabio 6 na kuvipanga katika safu zinazolingana, huku ukitalii njia zozote zile ambazo wanafunzi wanaweza kuzitumia katika kuvipanga vihesabio hivi.

Baada ya dakika tano, waache wanafunzi kwenye vikundi washirikishane njia walizozigundua za kuweza kupanga hii namba 6. Kagua ili kwamba angalau kikundi kimoja kiwe kimejumuisha mpangilio kwa safu moja tu. Waambie wajaze namba 6 katika jedwali lao kama inavyooneshwa katia Nyenzo Rejea 2 .

Kisha, waache wajaribu namba12 lakini, kabla ya kupanga, lazima wabuni idadi ya mipangilio inayoweza kutokea, na kisha wakague kama waliyobuni ni ya kweli.

Rudia kwa kutumia namba zote za kwenye jedwali.