Somo la 2

Katika sehemu hii, tunaendeleza kazi iliyopita ya namba sehemu katika michoroti kwa kuongeza namba rahisi za sehemu za kujumlisha na kutoa.

Unapofundisha, jiulize maswali haya mwenyewe:

Unalazimika kuwasaidia sana wanafunzi wako? Kama ndiyo, kwa nini unafikiri hivi ndivyo?

Je, wewe na wanafunzi mnafurahia shughuli za vitendo/?

Unafikiri wanafunzi wanajifunza zaidi kwa njia hii kuliko kama ungekuwa umewaambia tu? Unajuaje?

Uchunguzi kifani ya 2: Kazi zaidi za michoroti ya namba sehemu

Bwana Umaru alileta kwenye somo lake mchoroti wenye idadi kubwa ya hesabu za sehemu za kumi alizoandaa na kumwambia kila mwanafunzi atengeneze mchoroti kama huo kwa kutumia nyenzo alizowapatia. Baada ya dakika 15, aliwasaidia wanafunzi ili watumie michoroti yao ya namba sehemu ili kutafuta majibu ya maswali yafuatayo:

8/10 ni kubwa zaidi ya 5/10 kwa kiasi gani?

Nini tofauti kati ya 8/10 na 5/10?

8/10 - 5/10 ni ngapi?

Aliandika jibu la 8/10 - 5/10 = 3/10 ubaoni na kuwaambia wanafunzi wanakili hesabu hii kwenye madaftari yao.

Baadaye aliwaambia wanafunzi wake wafanye kazi wawili wawili na wafanye hesabu kadhaa za kujumlisha sehemu za kumi kwa kutumia michoroti yao ya namba sehemu. Alizitafutia majibu kadhaa, na kisha kuwaambia wale waliokuwa wanafanya vizuri kutafutiana majibu.

Bwana Umaru alishangazwa na kile ambacho wanafunzi waliweza kukifanya, lakini pia aling’amua kuwa alihitaji kuwapa wanafunzi mazoezi zaidi na muda zaidi wa kutoa mawazo yao kadiri walivyokuwa wanafanya kazi.

Shughuli ya 2: Kujumlisha na kutoa namba sehemu rahisi

Kabla ya somo, andaa maumbo duara matatu – duara kamili, robo duara na nusu duara, kila moja likiwa na robo zote zilizooneshwa (angalia Nyenzo-rejea 3: maumbo duara ya namba sehemu).

Shika duara la robo, kisha la nusu na waulize wanafunzi wako wakuambie jibu iwapo utajumlisha maumbo duara haya mawili. Wape muda wa kujibu, na utakapopata jibu sahihi, andika jawabu ubaoni: ¼ + 2/4 = ¾

Kisha, shika maduara yote matatu na waulize jawabu litakuwa nini kama maduara yote yatajumlishwa pamoja.

Kama awali, subiri jibu sahihi na kisha andika jawabu ubaoni: 1 + ¼ + 2/4 = 1 ¾

Sasa wapange wanafunzi wako wawili wawili, na waambie wachore maumbo duara kama hayo ya sehemu za theluthi. Waambie waandae majibu ya kujumlisha ya kuwapatia wenzao na kuandika jawabu lote la kila swali.

Wakiwa wanafanya kazi, zungukia darasa na toa msaada panapohitajika. Ikiwezekana, waache wajaribu namba sehemu nyingine ili kuona kama kweli wameelewa wazo hili.

Weka baadhi ya vielelezo tofauti tofauti vya namba sehemu ukutani.

Unaweza kufanya shughuli hii kwa vipindi viwili ili kuimarisha ujifunzaji wa wanafunzi