Nyenzo-rejea ya 1:  Kukusanya na kutengeneza maumbo na violwa

Nyenzo ya Mwalimu kwa ajili ya kupanga/kurekebisha na kutumia na wanafunzi

Utahitaji kuchora/kutengeneza vipande vya kadibodi za maumbo ya P2 yafuatayo:

Pembetatu Mraba

Pentagoni/Pembetano Pembesita

Pembesaba

Pembenane

Sasa unaweza kuchunguza violwa vya P3

Kijisehemu hiki ni kwa ajili ya kutia gundi ili kuunganisha au kufunga umbo pamoja

Vilevile, unahitaji kukusanya au kutengeneza violwa vya P3:

Tufe

Mchemraba (mfano, kibonge cha sukari, au mchemraba uliotengenezwa kutokana na njiti za kiberiti)

Miche mstatili (mfano, boksi la kiberiti, boksi la viatu)

Koni (unaweza kukata kutoka sehemu nyingine na kuchomeka kwenye wavu wa koni uliopo hapa)

Micheduara (vibiringisho vya karatasi za chooni, msokoto wa kipande cha karatasi kilichoshikishwa kwa gundi).

Aidha, unaweza kutengeneza michemiraba, mapiramidi au micheduara kwa kutumia karatasi au mirija.

Nyenzo-rejea ya 2: Picha ya piramidi