Nyenzo-rejea ya 2: Saa za maji – njia za kupima muda katika historia

Taarifa za msingi/welewa wa somo wa mwalimu

Saa za maji zilikuwa ni moja ya vitunza muda vya zamani ambavyo havikutegemea uchunguzi wa vitu vya angani. Moja wapo za zamani kabisa ilipatikana kwenye kaburi la mmoja wa mafarao wa Misri Amenhotep I, aliyezikwa kama miaka 1500 BCE. Baadae iliitwa clepsydras (wezi wa maji) na Wagiriki, ambao walianza kuzitumia kama miaka 325

BCE, hivi vilikuwa ni vifaa vya mawe vyenye pande zilizoinama ambazo ailiruhusu maji kuturirika kwa karibu kiwango kile kile kutoka kwenye shimo dogo karibu na sehemu ya chini. Vifaa vingine vilikuwa ni chombo cha kisilinda au chenye umbo la bakuli kilichoandaliwa kujazwa taratibu na maji yanayotiririka kwa kiasi kili kile. Alama zilizoko ndani ya nyuso zilipima ‘masaa’ kulingana na kiwango cha maji kilivyokuwa kinazifikia.

Saa hizi zilitumika kutambua muda wakati wa usiku, lakini zinaweza kuwa zilitumika mchana pia. Aina nyingine ilikuwa na bakuli la metali lenye tundu kwa chini, lilipowekwa kwenye chombo cha maji, bakuli lilijaa na kuzama kwa muda fulani. Hizi zilikuwa bado zinatumika Afrika ya Kaskazini karne ya 20.

Saa za maji nzuri zaidi zilitengenezwa kati ya miaka ya 100 BCE na 500

CE na watengeneza saa na majusi wa Kigiriki na Kirumi. Huu ufundi ulioongezewa ulikusudiwa kutengeneza mtirirko wa maji uwe imara zaidi kwa kurekebisha msukumo na kutoa mwonekano wa ubunifu wa kupita kwa muda. Baadhi ya saa za maji zilipiga kengele, nyingine zilifungua milango na madirisha kuonyesha maumbo madogo ya watu, au zilitembeza mishale, mizunguko na mifano ya unajimu ya ulimwengu. Katika Mashariki ya Mbali saa za unajimu za mashine zilitengenezwa kutoka 200 hadi 1300 CE. Karne ya tatu ya clepsydras ya Kichina iliendesha mitambo mbalimbali ambayo ilidhihirisha jambo la kimajusi. Moja kati ya minara ya saa mizuri ulijengwa na Su Sung na wenzake mwaka 1088 CE. Mitambo ya Su Sung ilihusisha mnara uliokuwa ukiendeshwa kwa maji uliogunduliwa kama miaka 725 CE. Mnara wa saa wa Su Sung, ukiwa na urefu wa zaidi ya futi 30 ulikuwa na kifaa cha shaba nyeusi kilichokuwa kikiendeshwa kwa nishati kwa uchunguzi, kifaa cha anga kinachozunguka chenyewe, na paneli tano za mbele zenye milango inayoruhusu kuangalia mabadiliko ya kibete ambacho kiligonga kengele, na kushikilia kibao kilichoonyesha saa au muda mwingine maalumu wa siku. Kwasababu kiwango cha mtiririko wa maji ni kigumu sana kukisimamia kwa uhakika, saa iliyotegemea maji hayo isingeweza kuwa sahihi k abisa. Watu walijikuta wakijihusisha na mbinu nyingine.

Katika klepsidra ya Ctesibius kutoka karne ya tatu K.K, mshale wa saa wenye umbo la mtu ulipanda kulingana na maji yalivyoingia. Kutoka nje kwa maji kulisukuma mfuatano wa gia uliizunguka silinda yenye urefu wa saa sawasawa na kila tarehe ya siku

Chanzo Asilia: Inventors About.com, Website

Nyenzo-rejea ya 1:Njia zilizotumika kupima muda zamani

Nyenzo-rejea ya 3:Saa za vivuli