Nyenzo-rejea ya 3:Saa za vivuli

Taarifa za msingi/ welewa wa somo wa mwalimu

Wamisri mwanzo kabisa waliigawa siku yao katika sehemu kama sisi. Obeliski (majengo ya kumbukumbu yenye sehemu nne, membamba, yaliyochongoka) yalijengwa mapema kama miaka 3500 BCE. Vivuli vyake vilivyotembea vilitoa aina fulani ya saa za vivuli, kuwawezesha watu kuigawa siku kuwa asubuhi na jioni. Majengo haya pia yalionyesha siku ndefu zaidi na fupi sana za mwaka wakati kivuli mchana kilikuwa kifupi zaidi au kirefu zaidi. Baadae, alama ziliongezwa kuzunguka shina la jengo kuonyesha sehemu zaidi za muda.

Saa nyingine ya kivuli ya Kimisri, yawezekana kuwa ni ya kwanza ya kubebeka, ilianza kutumika kama 1500 K.K Hiki kifaa kiligawa siku ya jua katika sehemu kumi na sehemu mbili za utusiutusi wa asubuhi na jioni. Wakati shina refu, lenye alama tano, liliekekezwa mashariki na magharibi asubihi, kivuli cha mwamba ulioinuka upande wa mashariki kiliziangukia alama. Mchana, kifaa kiligeuzwa ili kupima saa za mchana..

Ulaya katika kipindi cha miaka ya 500CE hadi 1500 CE maendeleo ya teknolojia yalipungua. Mitindo ya saa za vivuli iliibuka, lakini haikwenda mbali na ile ya Misri.

Chanzo Asilia: Inventors About.com, Website

Nyenzo-rejea ya 2: Saa za maji – njia za kupima muda katika historia

Nyenzo rejea 4: Vizio vya muda