Nyenzo-rejea ya 4: Modeli za Mimea

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Kabla ya shughuli hii, watake wanafunzi wako kuleta vipande vya takataka/mabaki. Kusanya takataka pia. Vipande vya takataka/mabaki ni kama: bati; kadibodi; uzi; tepu; mabua; chupa plastiki; nguonguo; karatasi; nyavu; waya.

Hatua 1: Ligawe darasa lako katika vikundi vidogovidogo vya watatuwatatu au wannewanne. Andika maelekezo yafuatayo kwenye ubao au kipe kila kikundi kadi ya maelekezo:

Zungumzia mmea ukoje.

Kisha unda modeli za mimea kwa vipande vya takataka.

Hatua 2: Vipange vipande vya takataka ili kila kikundi kipata kiasi cha kutumia.

Hatua 3: Wape wanafunzi wako muda wa kupanga na kuunda modeli zao.

Hatua 4: Watake kila kikundi waje mbele ya darasa kwa zamu waeleze modeli zao kwa darasa.

Jinsi somo lilivyomwendea Frida

Modeli za mimea ambazo wanafunzi walitengeneza zilionesha kuwa wanajua muundo wa msingi wa mmea, lakini hawakuwa na hakika sana kuhusu sehemu mahususi kama vile gome, matawi ya pembeni na majani yalipo kwenye matawi.

Aliamua kuwapa nafasi waangalie mimea nje na kisha kurudi na kubadilisha modeli zao au kuziongezea. Wanafunzi wake walijua istilahi kiasi lakini hawakuzijua za kutosha kwa Kiingereza au lugha-mama yao, kwa hiyo walitumia mchanganyiko wa lugha hizi mbili. Kulikuwa na mimea ambayo hawakuijua majina yao kwa lugha zote mbili.

Modeli za wanyama zilizotengenezwa na wanafunzi kutokana na takataka
Mjusi - Imetengenezwa kutoka kwenye waya na shanga – yaonesha wanafahamu mwili mrefu ulio bapa – umbo lenye mkao wa S – miguu iliyoelekea upandeni – mdomo wazi, tundu za pua na macho makubwa upandeni, bila masikio 

Chura - Imetengenezwa kutokana na udongo wa mfinyanzi wa mtoni. Mwili mfupi wa kuchuchumaa, hakuna mkia, miguu ya nyuma yenye nguvu, miguu ya nyuma ya wavu, miguu mifupi ya mbele isiyo na

wavu, mdomo mpana, macho makubwa yaliyotokeza, ngozi laini

Mdudu – Chungu - Imetengenezwa kutokana na waya iliyotupwa. Sehemu tatu za mwili: kichwa, kidari, tumbo. Miguu 3 yenye pingili, mdomo, macho makubwa, kiwiko chenye papasi, Kiuno kati ya kidari na tumbo.Ndege - Imetengenezwa kutoka kwenye udongo wa mfinyanzi, waya, mbawa za kadibodi na manyoya ya karatasi, macho na tundu za pua zilizochorwa, shingo ya kijiti. Sifa za kawaida za ndege zimeoneshwa. Mfano: Ukucha uliokunjiwa nyuma kwa ajili ya kushika.

Nyenzo-rejea ya 3: Sifa-pambanuzi za kawaida za viumbe hai

Nyenzo-rejea ya 5: Mifano ya ujenzi wa wanyama ya wanafunzi kutokana na mabaki mbalimbali