Somo la 1

Nini kinafanya mimea iwe ya pekee? Vitu viwili, karibu mimea yote hutengeneza chakula chake kutokana na maji na gesi-kaboni dayoksaidi. Sehemu ya kijani ya mmea, klorofili, hufyonza nishati ya jua ili kutengeneza nguvu/nishati yenye kabohaidreti. Wakati huohuo, mimea huachia oksjeni. Binadamu na wanyama wasingeishi kama hakuna mimea. Ndiyo maana tunatakiwa tuitunze mimea kwa uangalifu!

Sehemu nzuri ya kuanzia kutafiti mimea ni kuchunguza baadhi ya mimea isiyotoa maua. Mimea ya kawaida haina maua, poleni au mbegu; huzaliana kwa njia tofauti. Kundi hili la mimea hujumuisha mimea ya kuvu na mwani. Nyenzo 1: uchunguzi wa mimea una taarifa zaidi kuhusu aina hii ya mimea.

Una mifano halisi ya mimea hii katika eneo lako?

Katika matembezi yako ya kawaida, jaribu kutafuta mifano ya mimea hii: hii itajenga mwanga katika kuibua maswali na wanafunzi wako. Unaweza kukusanya baadhi ya mimea na kupeleka darasani kwako.

Uchunguzi kifani 1 Inaonesha namna mwalimu mmoja alivyowahamasisha wanafunzi wake kuchunguza mimea na shughuli 1

Inaonesha namna unavyoweza kuwasaidia wanafunzi wako kuuliza maswali yao juu ya mimea ya aina hii.

Uchunguzi kifani ya 1: Mimea asili isiyotoa maua

Karume na wanafunzi wake nchini Tanzania walitembea kuzunguka eneo la shule yao wakitafuta mifano ya mimea isiyotoa maua. Walipata kuvu na mimea inayoota kwenye mashina ya miti na mawe. Waliiangalia mimea hiyo iliyoota nyuma ya mashina ya miti na mawe yasiyofikiwa na jua. Waliona mimea midogomidogo inayoota kwenye nyufa za nyumba karibu na tenki la maji ya mvua. Walichora kila mmea na kuonyesha sehemu inapoota. Wakiwa darasani, Karume aliwataka wanafunzi kufikiri kuhusu namna mimea hii inavyoweza kuzaliana. Aliweka mawazo yao yote kwenye maandishi kuzunguka darasa.

Kutafiti zaidi, wanafunzi walikusanya baadhi ya mimea (kuvu) na kuiotesha chini ya chupa safi ya plastiki. Baada ya muda fulani, waligundua kuwa, mimea ilitengeneza ganda la kijani ambalo lilibadilika kuwa la hudhurungi na kugawanyika kutoa mbegu. Walijadili kama mbegu hizo zingeota kufanya mmea mpya (kuvu).

Halafu wanafunzi walirudi kuchunguza mimea hiyo. Waligundua kwamba mimea hiyo ilikuwa na ganda lililokauka (rangi ya hudhurungi) kwa upande wa chini yake. Waliendelea kuchunguza mimea hiyo, lakini hawakuona mbegu. Karume alimwomba mwalimu wa bailojia kuwaambia zaidi juu ya mimea hiyo na jinsi inavyozaliana. Aliridhishwa na nama shughuli hii ilivyoongeza uelewa juu ya mimea.

Shughuli ya 1: Kuuliza maswali

Alge wa maji yasiyo chumvi ni mimea inayo tengeneza chakula na kutoa oksijeni. Otesha baadhi ya alge darasani kwa kufanya maji yabadilike kuwa kijani katika glasi wazi (au kusanya baadhi ya alge).

Wahamasishe wanafunzi, wakiwa katika makundi kuwaza maswali ya kuuliza juu ya alge. Nini wangetaka kukijua kuhusu alge? Wakumbushe wanafunzi tabia saba za viumbe hai. Inahitaji mwanga kukua? Inatoka wapi? Kwa nini ni muhimu? Kila kundi la wanafunzi waandike kila swali kwenye kipande cha karatasi.

Watake wanafunzi kubadilishana maswali. Weka maswali katika makundi yanayofaa kwenye ukuta wa darasa na kuyajadili. Maswali gani unaweza kuyatafiti? Vitu gani unahitaji kusoma kwenye vitabu, kuuliza wataalamu au kutumia mtandao? Maswali gani yanaweza kuwa magumu kuyapatia ufumbuzi?

Kama una muda wa kutosha, watake wanafunzi kufanya utafiti (rejea Nyenzo muhimu: kutumia utafiti darasani) na fanya uchunguzi kujibu baadhi ya maswali.

Sehemu ya 2: Uchunguzi makini wa mimea