Somo la 2

Sehemu muhimu ya kufikiri kisayansi ni kutafuta sampuli na kufanya uchunguzi. Mmekuwa mkichunguza mimea inayozaliana bila kutoa maua, mbegu au poleni. Lakini mimea mingi kwa sasa kutoka nyasi ndogondogo hadi mimea mirefu, ina maua ambayo hutengeneza poleni na hutoa mbegu zilizo kwenye ovari. (Angalia nyenzo rejea 2: kuzaliana kwa mimea itoayo maua kwa taarifa zaidi.)

Katika shughuli 2 unafanya kazi na wanafunzi kutafiti tabia za kufanana za mimea itoayo maua na jaribu kutoa ufumbuzi-namna gani kila mmea unachavua? Katika aina ya shughuli hii, wanafunzi wako watahusishwa katika kutafiti, kubadilishana na kuboresha mawazo yao.

Ni muhimu kwa wewe na wanafunzi kusikiliza kwa makini kila wazo na usidharau kile mmoja anachochangia. Majadiliano yatoe changamoto katika mawazo, siyo mtu-vinginevyo wanafunzi hawata furahia kazi ya aina hii.

Kufuatia shughuli hii, unaweza kuhitaji kuanza na orodha ya mimea asili itoayo maua. Unaweza kutumia kijitabu kutunza kumbukumbu kwa marejeo ya baadaye, pamoja na michoro na sampuli zilizokaushwa na kuhifadhiwa. Wanafunzi wengine na wazazi wanaweza kufurahia kukiangalia kitabu hiki na kuchangia mawazo yao.

Uchunguzi kifani 2 kinaonyesha namna mwalimu alivyowahamasisha wanafunzi kufikiri kuhusu utegemezi wetu kwenye mimea na kutafiti juu ya mimea tofauti inayotumiwa katika maeneo yetu.

Uchunguzi kifani ya 2: Mimea inayotumika kama kinga (ua)

Mutakyahwa aliandaa shughuli ya darasa katika siku za mapumziko. Aliwataka wanafunzi kutoa mrejesho wa mifano ya mimea waliyoipata (iliyo kufa au hai) inayotumiwa kutengenezea kinga kwa namna fulani. Kinga huzuia vitu ndani au nje. Aliwaambia kuwa wanaweza kuwahoji wazee kujua nini kilitokea zamani au kutafuta picha kwenye magazeti ya zamani.

Muhula uliofuata, wanafunzi walitoa mrejesho ya kile walichokipata. Mwalimu Mutakyahwa alifurahishwa na tafiti zao na wanafunzi walishangazwa na sampuli nyingi tofauti tofauti. Walipata mifano ya mihekia na wigo za miti; pia wigo uzuiao upepo, mimea inayotambaa na kutoa kivuli, wigo za mianzi na mapazia ya vitambaa vya nguo za pamba. Mutakyahwa alikusanya mawazo yao kwenye bango katika ukuta wa shule. Baadhi ya wanafunzi walileta michoro, hiyo ilikuwa na rangi mchanganyiko na inayojieleza vizuri.

Alitumia onyesho hilo kama sehemu ya kuanzia kwa majadiliano ya darasa juu ya faida na hasara za kutumia mimea kama kinga.

Shughuli ya 2: Umbo la maua

Wapange wanafunzi katika jozi, au makundi ya wanafunzi wanne kama una wanafunzi wengi. Litake kila kundi kutafuta ua ambalo huota katika mazingira yao.

Sasa, kila jozi itafiti kila kitu wanachoweza kuhusu umbo na kazi za ua walilochagua. (angalia Nyenzo rejea 2 kwa taarifa zaidi juu ya kuzaliana kwa maua.

Tumia maelekezo na maswali yafuatayo kama kiongozi kwa wanafunzi wako.

Chora umbo la ua

Weka lebo sehemu za maua. (kuwasaidia kufanya kazi hii, unaweza kuweka ubaoni mchoro mkubwa wa ua wenye lebo unayotaka waitumie

Elezea kazi za kila sehemu

Jinsi gani mmea unachavushwa: wadudu wanatembelea mmea huo? Je chavuo huwekwa kwenye stameni nje ya ua? Ni eneo lenye upepo?

Kila kundi likiwa tayari, wanawezakufanya mawasilisho ya maelezo darasani kuhusiana na dondoo zote za hapo juu