Somo la 1

Mfumo ikolojia ni mpangilio wa maisha na mwingiliano kati ya viumbe hai katika aina ya eneo maalumu. Hii ingeweza kuwa dimbwi, mto, ua wa miti iliyooteshwa, mti, msitu, uso wa mwamba au hata shamba. Inaweza kuwa ndogo kama maisha chini ya gogo linalooza au kubwa kama maisha ziwani.

Kufikiria juu ya mfumo ikolojia hakutakiwi kuwa na ugumu kwako na kwa wanafunzi. Ni vizuri kama wanafunzi watakuwa na muda wa kuangalia na kuchunguza mifumo ikolojia mbalimbali. Inabi wapate uelewa wa jumla wa ‘nini kinakula nini’, idadi ya spishi mbalimbali na kuuliza baadhi ya maswali juu ya namna wanyama tofauti wanavyohusiana. Ni muhimu kuwapa wanafunzi muda wa kuyafikiria maswali wanayotaka kulliza, mara nyingi majadiliano mafupi katika makundi madogo yatawaongoza kupata maswali mazuri zaidi.

Uchunguzi kifani 1 unaonyesha namna mwalimu mmoja alivyowadokeza wanafunzi wake juu ya mfumo ikolojia wa mahali pale –dimbwi. Shughuli 1 inaonyesha jinsi ya kuanza uchunguzi wa muda mrefu wa mfumo ikolojia wa mahali hapo.

Uchunguzi kifani ya 1: Kuchunguza mzunguko wa chakula kwa kuangalia mfumo ikolojia

Shule moja ya msingi kambi ya makazi pembezoni mwa Nirobi, Kenya, iko karibu na dimbwi la asili. Mmoja wa walimu alipeleka darasa lake kutembea maeneo ya dimbwi hilo ‘kuangalia na kufikiri’.

Kutokana na rangi ya kijani iliyokuwa imetanda kwenye maji ya dimbwi hilo, waling’amua kuwa kulikuwa na mamiloni ya mimea ya algae na maelfu ya nyuzi za spairojira wakitengeneza chakula kwenye mwanga wa jua. Waliona mamia ya viluwiluwi, waliokuwa wakila algae. Nini kinaweza kuwa kinakula viluwiluwi? Sifiso alikuwa ameshaona viunzi vya mifupa ving’avu vya kerengende vikining’inia kwenye matawi ya mitete. Labda vyura kama kumi hivi waliishi kwenye dimbwi hili, wakila kerengende na wadudu wengine waogeleao. Nyoka wachache wenye rangi ya hudhurungi walikuwa wakionekana, na hawa, yamkini walikula vyura. Nsediswa alikuwa ameona mwewe mmoja akishuka chini na kukamata nyoka mdogo. Mwalimu aliandika uchunguzi wao kadri walivyokuwa wanatembea. Baadaye, wakiwa wamerudi darasani, walibadilishana mawazo na mwalimu na mwalimu aliyaandika ubaoni. Kila mtu alijadili namna wanyama na mimea walivyounganika katika mzunguko wa chakula. Wanafunzi walinakili mchoro wa mzunguko wa chakula wa mwisho uliokubalika kutoka ubaoni pamoja na piramidi ya idadi ya hii

(Angalia Nyenzo rejea 1: Mzunguko wa chakula ).

Shughuli ya 1: Kuchunguza mfumo ikolojia ya mahali hapo

Ongea na darasa lako juu ya wazo la mfumo ikolojia. Orodhesha idadi ya mifumo ikolojia inazoweza kupatikana karibu na shulel (angalia Nyenzo rejea 2: mfumo ikolojia wa mahali hapo ).

Ligawe darasa lako katika makundi na yaache kila kundi lichague mfumo ikolojia wake na kuuchunguza kwa kipindi chote cha mwaka kilichobaki. Kama kuna mfumo ikolojia mmoja tu unaofaa karibu na darasa lako, kila mtu anaweza kuuchuguza. Waandae wanafunzi kuachizana/kupeana zamu kwenye kuandika matokeo ya uchunguzi. Wahimize waulize maswali yahusuyo wanyama waishio pale na namna wanavyoweza kuhusiana wenyewe kwa wenyewe. Ni aina gani za viumbe hai wanategemea kuwaona na kwa idadi gani? Nini kinakula nini? Ni vipi idadi inaweza kubadilika kwa mwaka. Andika haya maswali na utabiri wake kwa matumizi ya baadaye.

Baadaye, tafuta muda wa kutembelea hayo maeneo na wanafunzi, kufuatilia utabiri wao. Hii inakuwa ni mpango endelevu wa kikundi. Tafuta muda kwa kila majuma/wiki chache kutembelea maeneo hayo na kuandika habari mpya. Kwa njia hii, ufahamu na uelewa wa wanafunzi utakua vizuri.

Makundi yangeweza kutunza kitabu au jarida kuandika kumbukumbu za uelewa wao wa jinsi vitu vinavyotokea mfumo ikolojia wao.

Kadri mradi unavyoendelea, fikiri juu ya uhusika wa wanafunzi-wanapata motisha kwa shughuli hii? Wanafurahia njia hii ya kujifunza?

Sehemu ya 3: Kuchunguza wanyama: wawindaji na wawindwaji