Somo la 3: Kuthamini uzoefu na maarifa ya asili

Inasikitisha, mengi ya elimu ya asili yanayohusika na mazingira yapo hatarini kupotea katika nyakati za kisasa. Labda shule za msingi nchini zingeweza kuchukua jukumu la kufufua moyo wa kuvipenda kwa kutafiti na kurekodi maarifa na ueleo huo.

Wanafunzi katika chuo cha ualimu waligundua kwamba George, mtu ambaye alifanya kazi kama bawabu, alikuwa rasilimali nzuri kutokana na maarifa yake ya kina kuhusu ulimwengu wa asili wa eneo hilo. Lakini ufahamu na uelewa wake wote ulikuwa kichwani mwake na pengine angekufa nao. Tazama Nyenzo 4: Elimu ya asili nchini kwa mifano ya baadhi ya mambo tuliyojifunza kutoka kwake. Unamjua mtu yeyote kama huyu? Wangeweza kuja kuzungumza na wanafunzi wako?

Tunahitaji kuhamasisha wanafunzi wetu kuwa wapenzi wa mazingira. Tayari tumeshatafiti thamani ya kuwapa wanafunzi muda wa kufanya uchunguzi wa kina wa mifumo ya ekolojia na spishi tofauti. Uchunguzi kifani 3 unaonyesha jinsi gani masomo yanaweza kusisimua ikiwa tutathamini elimu ya wanafunzi wetu na kuwaruhusu kufanya maamuzi kuhusu masomo yao wenyewe. Hapa, wanafunzi waliweza kuonyesha masomo yao kwa wengine na kuamua nini walitaka kutafiti zaidi. Fikiria kuhusu masomo ambapo ungeweza kuijaribu hii.

Uchunguzi kifani ya 3: Kujifunza kutokana na uzoefu

Bwana Chema, mhadhiri wa elimu ya sayansi alikatishwa tamaa kuona somo la darasa la 5 juu ya ndege ambalo kwa kweli halikufanikiwa vizuri. Waalimu wanafunzi walifuatishia mtaala na vitabu vya kiada vya kipindi hicho, lakini wanafunzi walionekana wamechoka. Kuangalia nyuma jinsi somo ilivyoshindwa kukamata hisia za wanafunzi, Bwana Chema na mwalimu mwanafunzi Ngodwane waling’amua kuwa mtoto yeyote wa miaka mitatu ambaye hajaanza shule, tayari angeshatambua kuwa ndege ana mbawa, manyoya na midomo migumu na kuwa kwa kawaida hutengeneza viota na hutaga mayai.

Baadaye, Bwana Chema na Ngodwane walipanga somo tofauti kabisa ambapo walijumuisha ubunifu (kama vile vipande vya kiota cha mbayuwayu kilichoharibika, manyoya, yai lililototolewa, tai mfu ambaye aligongwa na gari asubui ile karibu na shule) na picha za ndege wa kawaida. Waliviweka vifaa kwenye dawati la mbele na kuacha makundi ya wanafunzi yachague kitu na kuwaeleza wanafunzi wenzao walichokuwa wanakifahamu kuhusu kitu hicho. Wangeweza kutuambia nini kuhusu ndege?

Ni somo tofauti kabisa! Hatukuweza kuwazuia kuongea. Walikuwa na mambo mengi sana ya kuongoe.Walituambia mambo ambayo hatukuyafahamu, kama vile: mbayuwayu hujamiana maisha yao yote, huzaa watoto wachache kila msimu, na wakati mwingine, kwa vifaranga waliokufa hutupwa.

Nje ya kiota , unakuta vitu vinavyonyonya damu kama kupe wanaoweza kukimbia haraka sana. Wanafunzi waliendelea hadi muda wa kula mchana wakituelezea vitu vya kuvutia walivyojua kuhusu ndege wa mahali hapo na kujadili maswali yao wenyewe ambayo hayakujibiwa. Haya yaliandikwa kwa ajili ya kujibiwa baadaye. Kuona baadhi ya mifano ya ndege waliowajadili, angalia Nyenzo rejea 5: Ndege wa Tanzania .

Shughuli muhimu: Kutafiti na kutunza kumbukumbu za maarifa ya mahali hapo

Hapa, wewe na wanafunzi wako panga na chora jedwali kubwa kwenye bango kuandika taarifa ambazo wanafunzi watatafuta kuhusu aina zote za wanyama wa mahali hapo. Ingeweza kuwa na vichwa vya mihimili kama:

Jedwali limetengenezwa na linajazwa kwa muda fulani. Wahimize wanafunzi wako waongeze maswali kwenye jedwali. Kama inawezekana, tumia rangi tofauti kwa maswali na majibu. Sehemu wazi zitaonyesha maeneo yanayohitaji utafiti zaidi.

Unaweza kuwaambia wanafunzi tofauti wawajibike kuchunguza kuhusu wanyama mahsusi, lakini himiza kazi ya pamoja. Kama una darasa la rika tofauti, wanafunzi wakubwa wangeweza kuwasaidia wadogo kuandika kumbukumbu. Utahitaji kupanga muda kuwaruhusu wanafunzi waongeze majibu yao kwenye jedwali.

Mwishoni mwa muhula au mwaka, taarifa zinaweza kuhamishiwa kwenye kitabu kikubwa cha kutunza kama kumbukumbu kwa baadaye.

(Angalia Nyenzo rejea muhimu: Kutumia teknolojia mpya ni msaada wa kutafiti taarifa au kuonyesha taarifa).

Nyenzo-rejea ya 1: Mzunguko wa chakula