Somo la 2

Kuna ushahidi wa kutosha kwamba watu wote wa leo wametokea kwenye jamii moja ya watu iishio Afrika kama miaka 150 000 iliyopita. Hadi hivi karibuni, wanadamu waliishi maisha ya asili, wakiboresha teknolojia zilizofanya maisha yao rahisi na mazuri. Leo, teknolojia mpya zinatupa uwezo wa kuharibu dunia-na hata tabia ya hali ya hewa-kwa njia ya haraka.

Sehemu hii inaangalia jinsi unavyoweza kuchunguza pamoja na wanafunzi madhara tunayoleta katika dunia. Nini kinaidhuru? Na nini kinairejesha katika hali yake? Kuna mimea na wanyama wengi waliotoweka katika mchakato wa asili lakni shughuli za binadamu zinaweza kuchangia kupotea kwa baadhi ya wanyama na mimea. Hivyo, ni muhimu kuwasaidia wanafunzi kuelewa kuwa tabia yao inaweza kuleta madhala ya muda mrefu kwenye Dunia na mazingira.

Uchunguzi kifani 2 unatuambia namna mwalimu mmoja alivyotembea na wanafunzi wake kuamsha uelewa wa madhara ya binadamu kwa viumbe. Katika shughuli hii, ni muhimu kuchagua mada inayoendana na wanafunzi wako; Shughuli 2 inakusaidia kuongeza nyingine. Hii inaweza kuwa ni sehemu ya kuanzia mjadala, utafiti na utekelezaji. Wanafunzi wetu wanaweza kupanua kazi hii kuona jinsi matukio yanavyowasilishwa katika vyombo vya habari.

Jaribu kufanya tafiti za msingi mwenyewe kabla ya kuanza zoezi hili na wanafunzi wako. Ni viumbe gani wapo hatarini kutoweka katika nchi au eneo lako? Kama unaweza kupata mtandao, inaweza kuwa nyezo kuu kukusaidia ( Nyenzo rejea muhimu: Matumizi ya teknolojia mpya), lakini unaweza kuwaomba wataalamu, walimu wa shule za sekondari na wanajamii wengine kusaidia au kuja kuongea na wanafunzi.

Uchunguzi kifani ya 2: Kuongeza ufahamu wa wanyama waliohatarini kutoweka.

Preksedis Ndomba alikuwa akizungumza na wanafunzi kuhusu ndege asiyeruka waitwao dodo wa Madagaska. Huyu alikuwa ni ndege mkubwa aliyekuwa akila matunda yaliyoiva na kudondoka chini. Alijenga kiota chake ardhini kwa sababu hakukuwa na wanyama wala nyama kisiwani Madagaska. Halafu, mabaharia wengi walianza kutembelea kisiwa,

wakileta wanyama kama nguruwe, nyani na panya. Kwa miaka mingi, idadi ya dodo ilipungua na kufikia 1680 dodo wa mwisho alikufa.

Halafu, Ndomba alipanga wanafunzi katika makundi manne na kuwapa kila kundi kadi ndogo sita, kila moja ikiwa na moja ya:

Miti ya matunda iliyokatwa kupisha uoteshaji wa mazao mengine

Mabadiliko ya hali ya hewa na kuwa baridi mno kwa dodo

Watu zaidi huwinda dodo kwa chakula

Watu wengi wakichuma matunda kabla hayajaiva na kuanguka

Watu wengi kuwinda dodo kwa ajili ya manyoya

Wanyama wadogo walikula mayai ya dodo

Ndomba aliamuru kila kundi kusoma kadi na kupanga kwa mtiririko kuelezea kwa nini dodo alipotea. Aliwapa dakika ishirini kwa zoezi hili na wakati huo alizungukia kila kundi akiwauliza maswali juu ya ufahamu wao. Mwishoni, kila kundi liliwasilisha mawazo yake kwenye jedwali la darasa. Dhana iliyojitokea zaidi ni, kuliwa kwa mayai na Ndomba alihakikisha hili kuwa ni sababu kubwa kwa dodo kupotea.

Halafu, aliwauliza wanafunzi kama walisikia wanyama wengine waliohatarini kupotea. Wanafunzi walitaja tembo, chui, na wanyama wengine kwa hapa nyumbani kama kifaru na baadhi ya mimea. Waliamua kwa pamoja kuchunguza baadhi ya wanyama kupata sababu za wao kupungua. Waliandika barua kwa asasi zinazohusika na kuhifadhi mazingira kutafuta taarifa zaidi juu ya wanyama na kutengeneza mabango ya utafiti wao na kubandika ukutani (nyenzo rejea 4: Kifaru).

Shughuli ya 2: Kutengeneza karatasi la alama - ‘haribu’ dhidi ya‘saidia’

Tunafanya nini ulimwenguni? Katika shughuli hii, tumia swali hili kuongeza uelewa wa mambo ya mazingira ya ndani na nje ya nchi.

Tumia ukuta nyuma ya darasa kutengeneza jedwali kubwa-weka safu mbili. Andika safu moja ‘dhuru’ na nyingie ‘ponya’.

Kila juma\wiki, kundi tofauti la wanafunzi litakusanya magazeti ya wiki lililopita, sikiliza redio, au televisheni na kutafuta hadithi au picha inayoonesha namna watu wanavyoathiri mazingira. Unaweza kuwa na hadithi nyingi kuhusu uchomaji wa misitu, ufugaji kupita kiasi, utupaji ovyo takataka, upandaji miti, utengenezaji wa barabara mpya.

Wanafunzi watoe muhtasari wa hadithi kwa kutumia vichwa hivi: Kipi ni kichwa cha habari cha hadithi?

Ni sehemu gani za mazingira zimeathirika?(hewa, udongo, maji)

Zimeathirikaje? Ni madhara ya muda mrefu au ya muda mfupi? Nani anahusika/

Kundi linawasilisha hadithi darasani halafu linaongeza mchango wake kwenye safu husika.

Safu zikijaa, wanafunzi hupiga kura dhidi ya chaguo muhimu kwa kila safu na hizi zinajumuishwa kwenye ‘kinachotupa

wasiwasi-tunachopenada kuona’ marejeo ya baadaye.

Fikiri jinsi mawasilisho ya kundi yanavyoweza kuchangia kwenye tathmini ( Nyenzo rejea muhimu: Kutathmini mafunzo ).