Nyenzo-rejea ya 1: Nadharia ya asili ya binadamu ‘Kutoka Afrika’

Taarifa za msingi\ welewa wa somo kwa mwalimu

Wataalamu wengi wanaamini kwamba asili yetu ni homo sapiens,

aliyotokea Afrika, kati ya miaka 200,000 na 100,000 iliyopita. Hadi miaka

30,000 iliyopita Homo sapiens walikuwa wametawanyika sehemu zote ulimwenguni isipokuwa Amerika; walau hadi miaka 11,000 iliyopita, kila bara lilikuwa na watu isipokuwa Antaktika.

Homo sapiens walikuwa na zana nyingi zaidi ya watangulizi wao, ukijumuisha mawe yenye ncha kama wembe na zana za mifupa, miti na pembe za ndovu. Waliishi katika makazi makubwa na kulikuwa na mahusiano makubwa kati ya vijiji na makabila. Mawasiliano kupitia lugha ya maneno, sanaa, michoro ya mapangoni, sanamu na muziki yalikuwa muhimu kwa maisha ya binadamu. Baadaye, maendeleo ya binadamu- kilimo, ustaarabu, ongezeko kubwa la watu, viwanda na kukabiliana na mazingira-vimetokea kwa kipindi kifupi cha miaka 10,000.

Fuvu la reptilian wa zamani (miaka milioni 230-195 iliyopita)

Fuvu la mamalia (miaka milioni 54-16 iliyopita)

Fuvu la sokwe wa sasa

Fuvu la mtu wa sasa

Nyenzo-rejea ya 2: Udadisi wa kazi za sanaa