Nyenzo-rejea 3: Historia ya teknolojia

Taarifa za msingi\ welewa wa somo kwa mwalimu

Kabla hujasoma kuhusu historia ya teknolojia tumia dakika chache kufikiri namna teknolojia ilivyoanza. Unafikiri ilianza lini? Aina gani ya vitu watu wa mwanzo walihitaji kutengeneza? Unadhani ni kitu gani kinaweza kuwa cha kwanza kabisa kutengenezwa? Kwa nini?

Teknolojia ni kitu kilichotengenezwa kwa muda mrefu; kina umri kama ulivyo wa binadamu. Na ni kiini cha uzoefu wa watu wengi. Mara nyingi imekuwepo na itaendelea kuwepo.

Utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa maisha ya binadamu yalianzia Afrika; kusini mwa Afrika sasa kunafahamika kuwa ni makazi ya mwanzo ya watu wote-ni susu ya ubinadamu.

Kadri watu walivyoendelea hapa Afrika na kuboresha tamaduni zao, walipata njia za kutumia, kubadilika na kubadili vitu asili kufanya maisha yawe rahisi. Walianzisha mifumo ya kitamaduni na himaya. (Mifumo yenyewe ni aina ya teknolojia-njia ya kurekebisha maisha ya binadam na tabia zao.)

Labda ugunduzi muhimu wa kwanza ulikuwa ni mabegi, au vikapu, na mafundo ya kufungia vitu. Ngozi, sehemu za mimea, na nyuzi pengine zilitumika, na mafundo, kusuka na kusokota viligunduliwa. (Bila shaka, vibuyu, au kalabashi, viliweza kutumika kama vyommbo vya kuchukulia vitu, mabegi na vikapu yawezekana viligunduliwa na wanawake ili kubebea chakula walichokusanya, kusudi wabebe chakula kingi kuliko wanachoweza kuchukua mkononi. Pia walihitaji kuwa na uwezo wa kubeba watoto wao salama huku wakiwa wanakusanya mizizi, matunda na mazao.

Mara baada ya ugunduzi wa mabegi na vikapu, mikono ya binadamu ilikuwa huru kutumika kwa kazi nyingine. Uwindaji na zana nyingine zilibuniwa pia, kwa kutumia vitu vigumu kama mifupa na mawe. Mifupa mirefu iliweza kupindwa au kukatwa na kutengenezwa kwa kuisugua ili iwe na ncha kwa ajili ya kukatia au kuchomea.

Mawe yaligongwa na kuchongwa kufanya shoka za mawe. Mawe yenye ncha kali yaliweza kutumika kuchunia ngozi kupata ngozi. Zana hizi ziliweza kutumika kutengenezea zana nyingine. Na hivyo watu waliboresha zaidi na zaidi teknolojia kufanya maisha ya mwanadamu kuwa rahisi kwa namna moja-na labda magumu kwa wengine.

Kutoka enzi hizo, watu walianza kujiremba wenyewe. Walitengeneza vito kama shanga, heleni na mikufu ya kuvaa. Hivi vilihitaji ujuzi wa kiteknolojia.

Kabla ya hapo, wanadamu waligundua kuwa labda wangepata rangi fulani kutokana na mimea. Pia waligundua madini ya rangi mchanganyiko yaliyosagwa kufanya rangi asili za kupaka na kupamba miili yao. Kwa kukata ngozi na kwa kusugua kwa majivu katika vidonda, makovu mazuri ya kudumu yaliweza kutengenezwa. Katika nyakati zilizo fuata, michoro ya mwilini ilivumbuliwa.

Bila shaka, walipammba vitu na zana walizotengeneza. Tuna uhakika kuwa watu wa zamani walipenda uzuri na vitu vilivyotengenezwa kwa umaridadi.

Wakati fulani, udhibiti na matumizi ya moto ilikuwa ni sehemu muhimu ya maisha ya binadamu. Hii iliwawezesha watu kupambana na giza, na njia ya kutengeneza baadhi ya chakula kwa kupika au kufukiza moshi.

Udhibiti wa moto ulimaanisha kuwa watu sasa waliweza kuhama na kuishi sehemu za baridi kali. Moto pia uliweza kutumika kuchomea vyungu vilivyotengenezwa kwa udongo. Mchakato huu ulifanya vyungu viwe imara kiasi cha kutumika kwa kupikia na kuhifadhia vitu.

Ugunduzi jinsi ya kutafuta, kuchimba,kuyeyusha na kuumba chuma ilikuwa mwendelezo mwingine wa ugunduzi na uvumbuzi.

Ufugaji wa wanyama pia ni maendeleo ya kiteknolojia. Hii ilisababisha kuwe na maisha ya kutangatanga. Katika sehemu kame,watu walijifunza kuchimba visima ili kupata maji ya kuwanywesha wanyama. Wanyama wanaofugwa walikuwa ni alama ya utajiri. Biashara za kubadilishana vitu kwa vitu pengine ndipo zilipoanza.

Kujifunza namna ya kupanda mazao kulileta maendeleo ya kilimo na kilimo cha mahali pamoja. Udhibiti wa maji ya umwagiliaji ilikuwa ni teknolojia nyingine iliyogunduliwa.

Makazi yalibadilika kuwa vijiji. Vijiji baadae viliboreshwa na kuwa miji na majiji. Miji na majiji yalikuwa ni mifumo changamano yaliyohitaji kazi nyingi tofauti tofauti ambazo zilihitaji ujuzi na teknolojia fulani.

Kadili maisha ya watu yalivyokuwa changamano, zana nyingi na mifumo tofauti ilikuwa lazima ianzishwe. Zana zilitumika kuweka alama au kumbukumbu kwenye mawe au udongo ambazo zilikuwa na ujummbe au taarifa muhimu. Mifumo ya uandishi ilianzishwa.

Hatimaye, zana changamano na seti za zana zilibadilishwa kuwa mashine ambazo ziliweza kufanya kazi za watu au wanyama wengi. Ziliweza kufanya kazi ambazo hata binadamu hakuwa na uwezo wa kuzifanya hapo kabla. Watu walipogundua namna ya kutumia upepo na maji kama nishati za kuendeshea mashine, mfumo wa uzalishaji uliboreka. Matumizi ya makaa na mvuke ilikuwa ni maendeleo mengine ya teknilojia yaliyopelekea mapinduzi ya viwanda.

Unaweza kuona kuwa maendeleo ya teknolojia yana leta mabadiliko ya aina zote. Mara nyingine, mabadiliko ni mazuri na mara nyingine huweza kusababisha matatizo.

Leo tunaishi katika ulimwengu wa kisasa ambao umetawaliwa na mabadiliko ya haraka ya kiteknolojia. Je tunaidhibiti teknolojia au inatudhibiti sisi? Kufahamu matumizi ya technolojia na kuwa na uwezo wa kuishi na kufanya kazi kama binadamu katika ulimwengu wa kisasa ni ujuzi muhimu sana wa kimaisha kwa kila mmoja kujifunza.

Chanzo Asili: Chuo Kikuu cha Fort Hare

Nyenzo-rejea ya 2: Udadisi wa kazi za sanaa

Nyenzo-rejea 4: Kifaru mweusi