Nyenzo-rejea 4: Kifaru mweusi

Mfano ya kazi za wanafunzi

Vifaru weusi, Dicerosbicornis, ni wanyama wenye asili ya sehemu za mashariki mwa Afrika na kati, ikijumuisha Kenya, Tanzania Kameruni, Afrika kusini, Namibia na Zimbabwe. Ingawa vifaru hawa hujulikana kama ‘weusi’, kwa uhakika kabisa wana rangi ya weupe-kijivu.

Kifaru mkubwa ana urefu wa sm 143-160 mabegani na mita 2.86-3.5 kwa urefu. Uzito wake ni kuanzia kilogramu 800-1400, mwenye uzito wa

pekee hufika hadi kilo 1820, na majike huwa madogo kuliko madume. Wana pembe mbili kichwani zenye urefu wa sm 50 lakini zinaweza kufika sm140. Mara nyingine, pembe ndogo ya tatu huweza kuota. Pembe hutumika kwa kujilinda, kutishia na kuchimbia mizizi na kuvunjavunja matawi ya miti wakati wa kula.

Ngozi nene ya kifaru huilinda kutoka kwa miiba na nyasi zilizochongoka/zenye makali. Ngozi yake huhodhi kupe kama kaa ambao huliwa na ndege wanaoishi na vifaru. Vifaru wana matatizo ya kuona, hutegemea zaidi kusikia na kunusa. Wanamasikio makubwa yanayozunguka kama satelaiti kutambua sauti yoyote na pua kubwa inayonusa vizuri kugundua adui.

Vifaru weusi ni walamajani na hula majani ya mimea, matawi, majani yanayo chipua, miti ya miiba na matunda. Chakula chake husaidia kupunguza kiasi cha misitu, ambayo hupelekea nyasi nyingi kuota ambazo ni muhimu kwa wanyama wengine. Inajulikana kuwa huwa wanakula kiasi cha mimea 220 ya aina tofauti. Anaweza kuishi siku tano mfululizo bila kunywa maji wakati wa ukame. Vifaru weusi huishi eneo lenye nyasi, savana na kwenye misitu ya kitropiki.

Hutafuta chakula asubuhi na jioni. Hutumia muda wa mchana kupumzika, kulala na kugaagaa kwenye matope. Kugaagaa kwenye matope ni sehemu muhimu katika maisha ya ya vifaru wote. Inasaidia kupunguza joto mwilini wakati wa mchana na kuwalinda dhidi ya kupe. Kama matope hayapo kimbilio lao ni kuviringika kwenye vumbi. Kunywa maji ni kitu cha kawaida kwa mchana.

Vifaru ni wanyama wanaoishi kwa kujitenga isipokuwa wakati wa kujamiana. Majike na vifaru watoto mara nyingine hukusanyika katika makundi madogo kwa vipindi vifupi. Madume hawakusanyiki kama majike ingawa muda mwingine huruhusu uwepo wa vifaru wengine. Hawana makazi maalumu na mara nyingine huingiliana makazi. Ukubwa wa makazi hutofautiana na kipindi na upatikanaji wa maji na chakula. Kwa ujumla, wana makazi madogo na makubwa sehemu zenye chakula kingi na maji na kinyume chake kama maji na chakula havipo. Katika mbuga za Serengeti, makazi yana ukubwa kati ya km2 43 hadi 133, wakati Ngorongoro yanaukubwa kati ya km22.6 mpaka 44. vifaru imegundulika kuwa wa na eneo fulani ambalo hupenda kutembelea mara kwa mara, ambalo huitwa ‘nyumba’, kwa kawaida huwa ni sehemu iliyoinuka juu.

Vifaru wana sifa ya kuwa wakali sana. Kutokana na matatizo yao ya kutokuona vizuri, watacharuka kama wakihisi kuna kitu hatari. Wamegundulika kuvamia matawi ya miti na kuchimba vichuguu. Vifaru siyo wakali kwa vifaru wenzao, daima huwa na ukali wa kughilibu. Madume mara nyingine hupigana kwa kusukumana vichwa. Madume hukwepana kadili inavyowezekana. Majike siyo wakali wenyewe kwa wenyewe.

Kifaru katika malisho

Kwa sehemu kubwa ya karne ya 20, Vifaru wa weusi ‘continental black rhino’ ndio waliokuwa wengi kuliko aina nyingine zote. Yapata miaka ya

1900 kulikuwa na maelfu ya vifaru Afrika. Wakati wa sehemu ya pili ya karne ya 20, idadi yao ilipungua kutoka makadilio ya 70,000 mwishoni mwa miaka ya 1960 hadi kufikia 10-15,000 mwaka 1981. mwanzoni mwa miaka ya 1981 idadi yao ilipungua na kufikia 2,500 , na mwaka 1995 iliripotiwa kuwa idadi yao ni 2410 tu. Kulingana na ripoti ya mfuko wa kimataifa wa kusaidia kuhifadhi vifaru, idadi ya vifaru imeongezeka na kufikia 30610 mwaka 2003. Kutokana na ripoti ya Juni ya umoja wa uhifadhi mazingira, utafiti wa karibuni wa vifaru wa Afrika Magharibi uliohusisha maeneo ya savana, unaonesha kuwa baadhi ya aina fulani ya vifaru imetoweka. Vifaru weupe wa Afrika kaskazini nao wanakaribia kupotea kwa kuwa utafiti wa karibuni ulionyesha kupungua hadi wanne. Vifaru pekee walio ongezeka kiasi fulani ni vifaru weupe wa kusini mwa Afrika ambao idadi yao kwa sasa inakadiliwa kuwa 14,500 kutoka vifaru

50 kwa karne ilizopita. Vifaru weusi wamehatarishwa kutoweka kutokana na vitendo vya uwindaji haramu kwa ajili ya pembe na kuharibiwa kwa makazi yao. Pembe hutumika kwa madawa ya asili ya Kichina. Uhakika unaosemekana juu ya matumizi ya pembe za vifaru kutibu magonjwa haujathibitishwa na madaktari. Hitaji la pembe za vifaru lilivuma miaka ya

1970 na kusababisha idadi ya vifaru kupungua kwa asilimia 96 kati ya mwaka 1970 na 1992.

Habari zaidi juu ya vifaru weusi na shughuli nyingi na nyenzo za kutumia na wanafunzi shuleni zinaweza kupatikana kwenye mtandao www.savetherhino.org. [Tip: hold Ctrl and click a link to open it in a new tab. (Hide tip)]

Kuna mashirika mengi yanayohusika na uhifadhi wa mazingira Tanzania kama vile Mfuko wa kuhifadhi wanyama pori Afrika (African Wildlife Foundation) or the. au Mradi wa Tembo wa Tarangire (Tarangire Elephant Project). Yameorodheshwa na Mfuko wa hifadhi Afrika (African Conservation Foundation) www.africanconservation.org.

Nyenzo-rejea 3: Historia ya teknolojia

Nyenzo-rejea 5: Dhana wanayoweza kuwa nayo wanafunzi juu ya kufanya kazi katika makundi