Nyenzo-rejea ya 1: Rasilimali zinazorejelezwa na zisizorejelezwa
Taarifa za msingi/welewa wa somo wa mwalimu
Rasilimali zinazorejelezwa | Rasilimali zisizorejelezwa |
---|---|
Mbao kutoka miti ya kupanda inayokua haraka | Mbao kutoka miti asilia ya porini |
Mazao ya kupandwa | Mitishamba ikitumika kwa wingi sana kwa madawa |
Nyama kutokana na wanyama wa kufugwa | Wanyama mwitu wanaotishiwa kupotes |
Maji (kama hayakuchafuliwa) | Ardhi iliyomomonyolewa hairudi |
Hewa | |
RASILIMALI YA NISHATI | |
Nishati wa maji | Makaa ya mawe |
Nishati ya upepo | Mafuta |
Nishati ya jua | Petroli na dizeli ya mafuta |
Mafuta ya taa |
Kumbukumbu: unaweza ona jinsi mwalimu alivyokubali mapendekezo mengi toka kwa wanafunzi na walivyoweza jitahidi kutumia maneno yao wenyewe. Hili linawapa uwezo wa kujiamini zaidi na kuongeza mambo
mengine mengi. Kama mwalimu anasahihisha kila kitu kulingana na kitabu cha kiada hili litawavunja mori wanafunzi – kukubali na kufanya nao kazi kwa kutumua maneno yao ni muhimu sana.
Unaweza kuona pia jinsi mwalimu alivyoweka umuhimu juu ya mambo ya nishati – kwa kuongezea vipengele vidogovidogo. Ikitegemea wapi wanaishi, wanafunzi wanaweza kujua gesi asilia, ambayo ni rasilimali isizorejelezwa
Somo la 3