Nyenzo-rejea ya 1: Hadithi za sauti

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Ngoma inayomeza vitu

Msichana mmoja mdogo, mtoto pekee, alikuwa anaishi na wazazi wake katika kijiji fulani. Kutokana na hatari asizoambiwa, hakuruhusiwa kwenda mbali na wazazi wake pia hakuruhusiwa kucheza na watoto wenzake. Alijisikia kama mfungwa ndani ya nyumba yake na kutamani kuwa na uhuru kama watoto wengine.

Siku moja, alipata nafasi ya kutoroka wakati wazazi wake wakiwa wamelala baada ya chakula cha mchana. Mama yake alienda kufanya kazi shambani na mtoto akapanga kwenda kumshangaza hukohuko. Hakuwa na uhakika na njia ya kufika huko, na njia zinapokuwa mbili, anachagua njia ya bondeni kuliko ya mlimani.

Baada ya muda fulani anapita karibu na ngoma, inayojipiga yenyewe….

‘Bim! Bim! Bim! Mtoto mdogo! Mtoto mdogo! Rudi nyumbani!

Lakini mtoto ni mdadisi na anaendelea bila kujali. Karibu na kona nyingine anapita karibu na ngoma ya ukubwa wa kati inayojipiga yenyewe…

Bim! Bim! Bim! Mtoto mdogo! Mtoto mdogo! Rudi nyumbani! Lakini mtoto ni mdadisi na anaipita ngoma na kuendelea na safari yake.

Mbele zaidi, unafikiri ataona nini? Ndiyo, Ngoma kubwa inajipiga

yenyewe…..

‘Bim! Bim! Bim! Mtoto mdogo! Mtoto mdogo! Rudi nyumbani!

Hakika ni mdadisi, mtoto huyo alipuuza onyo hili pia. Njia inakaribia ukingoni mwa msitu na anapoingia katika msitu mnene miti inafunika nyuma yake. 

Hawezi kurudi nyuma tena-lakini kuna kelele za kutisha za ngoma katika msitu. Anakaribia kwenye sehemu wazi na anaiona ngoma kubwa kupita kiasi. Ni ngoma inayomeza-hatari ya kutisha ambayo wazazi wake waliogopa isije mkuta. Anamezwa na ile ngoma na kuangukia chini ya ngoma, watu wengine na wanyama wanamkimbilia na kumuuliza kama anakitu chochote kikali. Lakini hana. Anachoweza kuona anapoangalia juu anaona ufa wa mdomo wa ngoma na moyo mkubwa wa miti ukidunda…….

Ba-boom! Ba-Boom! BA-BOOM!

Wazazi wake nyumbani wanachanganyikiwa wanapogundua kuwa mtoto wao haonekani na kuona nyayo zake zilikoelekea. Baba yake analia na kujifunika kwa majivu ya moto. Lakini mama yake hatulii-anazunguka kijiji kizima kuazima vitu vyenye ncha kali na anakesha usiku mzima akiviweka kwa uangalifu kwenye nguo zake za ndani.

Siku inayofuata anaelekea msituni. Haoni ngoma zozote lakini anaingia msituni, miti inafunika kwa nyuma.

Anakaribia sehemu wazi na kuona ile ngoma inayoogofya na inayomeza, inauliza, ‘ndiyo! we mwanamke mnene! Unataka nini? Kabla hajaweza kujibu, alimezwa pia na watu walimkimbilia kumuuliza kama anavitu vyenye ncha kali. Lakini anahitaji kwanza kumwona mtoto wake na halafu anaonyesha vitu vyenye ncha kali. Wanaume ndani ya ngoma wanasimama kandokando ya ukuta wa ngoma na wanawake wanasimama kwenye mabega ya wanaume. Vijana wakiume wanapanda na vitu vyenye ncha kali na kuanza kuuchomachoma moyo wa mbao….

BA-BOOM! Ba- boom! Ba-boom, b-bm

Moyo unaposimama kudunda, wanatoboa njia ya kutoka nje ya ngoma, wanakimbilia kijijini kuomba msaada na ngoma hatari inayomeza watu inakatwakatwa vipande vipande. Watu katika kijiji kile walipata kuni nzuri za kutumia mwaka mzima.

Nyenzo-rejea ya 2: Mawimbi ya sauti- nyaraka za mwalimu