Nyenzo-rejea 4: Dhana ya kutathmini zana

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Imetengenezwa kwa kutumia nini? Ina muda gani?

Ina uimara gani?

Inahitaji kutunzwa sehemu nyeti? Inaweza kubebeka kirahisi? Unatengenezaje sauti?

Unafanya sauti kuwa ya juu? Ya chini?

Unatengenezaje sauti ya chini? Sauti kubwa? Ni rahisi kufanya? Unaweza kusikia sauti ya chini?

Nini kinatetema?

Ni rahisi kujifunza kupiga?

Inagharimu kiasi gani?

1. Chagua maswali muhimu wakati wa kutathmini zana. Tunashauri kuwa wanafunzi wachague vigezo/maswali yasiyozidi matano ili kutathmini kila zana.

2. Kwa kila vigezo au maswali waliyochagua, tengeneza mfumo wa vipimo vya alama chini ya 5. Alama za juu kwa kila zana itakuwa

25.

3. Kadili kila kundi linapowasilisha zana zake, wape alama kwa kila kigezo.

4. Alama hizi zinaweza kuandikwa ubaoni au kwenye karatasi gumu kubwa na kubandikwa ukutani

Kila kundi litoe hitimisho ya kazi yake kwa kusema: Alama kwa zana yetu ni:

zana yetu ni chaguo zuri kwa sababu..(ubora)

Zana yetu inaweza kuwa siyo chaguo zuri kwa sababu…(ugumu na matatizo ya zana).

Nyenzo-rejea 3: Dhana wanayoweza kuwa nayo wanafunzi juu ya kufanya kazi katika makundi

Nyenzo-rejea 5: Zana asili za muziki