Nyenzo-rejea ya 2: Njia salama za kuchunguza umeme

Taarifa za msingi/ welewa wa somo wa mwalimu

Waalimu wawili Dar Es Salaam wanajadili hatari na usalama wa umeme na mshauri wa kisayansi na wanaelezea kwanini wanaogopa kujihusisha na umeme darasani.

Aliwahakikishia kuwa betri za V 1.5 na balbu za mwanga tunazoona kwenye tochi ni salama kabisa.

Mwalimu mmoja anauliza: ‘Ni vipi umeme unakuwa hatari?’ Mtaalamu anaelezea kuwa umeme tunaotumia majumbani ni volti 220, hivyo una nguvu mara mia ya umeme wa betri. Nyaya zenye nguvu zinazobeba umeme nchi nzima zina nguvu mara maelfu zaidi.

Kwa hiyo waalimu waligundua kuwa wangeweza kuwa salama kufanya majaribio ya umeme darasani.

Mtaalamu aliwashauri wahakikishe kuwa wanawaambia wanafunzi ukweli wa hatari ya umeme, na aliwaachia baadhi ya mifano ya vitinyi/vipeperushi vya usalama vinavyopatikana mahali pale.

Waalimu hao wawili waliamua waangalie na kwenye magazeti ya pale, The Guardian, makala juu ya ajali zinazohusika na umeme na kuwafanya wanafunzi wao wajadili sababu na matokeo ya haya mambo yaletayo huzuni.

Nyenzo-rejea ya 1: Kuangalia balbu ya tochi kwa makini

Nyenzo-rejea 3: Dhana ya kutathmini zana