Nyenzo-rejea 3: Dhana ya kutathmini zana

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Muhutasari wa majadiliano kwa shughuli 1

Kuwa mvumilivu. Waache wanafunzi wako wajishughulishe. Kumbuka kuwa elimu ‘inayokuja kirahisi’ ‘huondoka kirahisi’. Usiwaingilie. Watajiamini na kuendelea. Mwishowe, wanaweza kufanya kazi kwa kubahatisha. Halafu watajaribu kuthamanisha hii na kuuliza: ‘Nini kinaendelea hapa?’

Utaona kuwa watoto wadogo sana watafikiri kuwa itawaka kama wakigusisha sehemu ya chini ya balbu ya tochi na sehemu ya juu ya betri, metali kwa metali. Wanashangaa sana wanapoona sivyo.

Wanafikiri, ‘Hapana! Lakini inahitaji baadhi ya nyaya! Au waya!’ Halafu wanaunganisha kipande cha waya wa kuunganishia kutoka upande wa chini wa betri hadi upande wa juu. Bado balbu haiwaki.

Tazama uone ni mbinu gani wanafunzi wako wataitumia.

Sehemu ya chini ya balbu ya tochi lazima igusane na sehemu ya juu ya betri upande wa balbu wa metali.

Mipangilio mitano

Wanaweza kuipata hii mipangili wao wenyewe, kwa kubahatisha. Wape muda na wahimize.

Kundi moja au mawili yanaweza kugundua kuwa balbu inawaka hata kama iko kwa pembeni .

Imetoka: Umthamo3, University of Fort Hare Distance Education Project

Nyenzo-rejea ya 2: Njia salama za kuchunguza umeme

Nyenzo-rejea 4: Kadi za kazi