Nyenzo-rejea ya 1: Ushauri wa Usalama kwa waalimu

Taarifa za msingi/ welewa wa somo wa mwalimu

Kutoliangalia jua

Ni muhimu uwatahadharishe watoto wasiliangalie jua moja kwa moja. Waambie kuwa macho yetu yana lenzi zilizojengewa zinazofanya kazi kama miwani ya kukuza vitu. Utaangalia JOTO na nguvu ya mwanga kutoka kwenye jua mpaka nyuma ya mboni ya jicho na retina vinavyotusaidia kuona. Joto hili linaweza kuunguza na kuteketeza moja kwa moja seli za retina, kama vile miwani ya kukuza vitu inavyoweza kuunguza na kuteketeza karatasi. (Kwa kutumia vitu kama viona mbali/darubini inaweza kuwa mbaya zaidi). Waambie kuwa hakuna mtu anayetakiwa kuthubutu kucheza na jinsi ya kuona.

Usiungue

Vyanzo vingi vya mwanga wa moja kwa moja pia huhusisha joto kali. Wadudu tu kama vimetameta na aina fulani ya minyoo wanaonekana kuzalisha mwanga bila joto. Wasimamie wanafunzi kwa uangalifu wakati miale ya moto inapohusika. Pia, hakikisha kuwa viberiti vimehifadhiwa vizuri na vimetumika ipasavyo.

Mshtuko wa umeme

Tahadhari zote muhimu inabidi zichukuliwe pale vifaa vya umeme darasani kama vyanzo vya umeme. (Hakuna nyaya zilizokatika, muunganisho mbaya, plagi ziwe zimewekwa vizuri na hakuna maji jirani na umeme)

Mwisho, si vizuri kufikiri juu ya mwanafunzi kujeruhiwa, kuunguzwa au kuumizwa, bali hakikisha umefikiria uwezekano kwamba linaweza kutokea kwako au mwenzako, na jiandae kuchukua hatua za huduma ya kwanza

Nyenzo-rejea ya 2: Vivuli vya Ukutani