Nyenzo-rejea 4: Shughuli za ziada za uakisi

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Ni kweli kwamba tuna sura mbili?

Je, sehemu mbili za uso wetu ziko sawa? Wanafunzi watafurahia shughuli ambapo unaangalia picha kamili uliyoleta au waliyoleta.

Simamisha kioo kidogo cha mkononi katikati ya uso kwenye picha ili nusu iliyoakisiwa itengeneze uso mmoja na nusu ambayo haijakingwa. Sasa fanya hivyo hivyo kwa upande wa pili. Haishangazi namna sura hizi mbili zinavyotofautiana? Hii ni kwa sababu nyuso zetu hazilingani.

Kushika mkono usio sahihi

Jaribu kuushika mkono wa taswira yako kwenye kioo kikubwa-ukishika mkono wa kulia, itakupatia picha ya mkono wake wa kushoto.

Rudia zoezi hili, lakini mara hii, panga vioo viwili katika pembe sawa. Angalia kwenye kona utaona taswira yako moja. Fanya kama unashika mkono taswira zilizoko kwenye kioo.

Ni mkono upi ambao taswira zimeutoa safari hii? Unaweza kutafuta ni kwa nini hili linatokea? Kutumia uakisi

Tafakari matumizi ya vioo: Ni vifaa gani vina vioo?

Ni wapi vinapotumika?

Ni jinsi gani vioo vinaweza kutumika dukani kusaidia ulinzi? Uakisi wa kutisha

Fanya majaribio kwa kuangalia kwenye uakisi kwenye vipande vilivyopinda vya chuma kama vijiko na birika la umeme.

Hutokea nini kwenye uakisi?

Ni mfumo gani unaougundua?

  • Mwanga na giza
  • Kusanya pamoja vifaa na zana tofauti zinazong’aa. Jaribu kuziangalia:
  • Kwenye mwanga wa kawaida wa darasani;
  • Kwenye ‘kisanduku cheusi’ ambako kuna mwanga hafifu; Wakati tochi imewashwa kuvimulika.

Ni vitu gani vinang’aa zaidi? Unaweza ukavipanga kufuatana na mng’ao wake? Hutokea nini ukiviweka vitu hivyo kwenye sanduku? Hutokea nini ukivimulika na tochi? Unaweza kuona mfumo wowote kwenye uchunguzi wako?

Nyenzo-rejea 3: Habari juu ya mwanga

Nyenzo-rejea ya 5: Mawazo ya namna ya kutengeneza kivuli cha kikaragosi