Nyenzo-rejea 3: Jua, Mwezi na Maji

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Unajua, samakigamba, pweza, samaki kipepeo, makundi ya sadini na ya samaki aina ya bangala, papa mwenye meno makali na nyangumi. Kajenge zizi kubwa na nitakutemebelea kwa furaha, tena na tena; hivyo ndivyo nitakavyofanya’ alisema jua. Na alianza kufanya kazi mara moja n aalijenga vibanda vingi vikiwa vimezungukwa na uzio, zizi, ambalo lilienea pande zote kulingana na macho yalivyoweza kuona.

Pale zizi kubwa lilipokamilika, jua alipeleka mwaliko wake kwa maji. Hatimaye yeye na mke wake, mwezi waliona maji yakija. Kwa mbali waliyaona maji yajikatisha kwenye miti na vilima hadi, mwishowe

yakazunguka kwenye vifundo vyao vya miguu‘ nimekuja jua mpendwa, nina furaha sana kuwa hapa na kumwona mkeo. Umeniandalia sehemu kubwa na nzuri sana. Hata maji yalipokuwa yakiongea,jua na mwezi maji yenye samaki wakubwa na wadogo yalikuwa kwenye magoti“Una uhakika una vyumba kwa ajili yetu sote?” maji yaliuliza, “ kwa kuwa hatujafika wote bado’ ninavyo’, jua lilitabasamu. Bila wasiwasi mwezi ulutoa mwanga. Lakini wakati wakiongea haya jua na mwezi walikwea sehemu

juu kabisa mwa paa lao wakati samaki warukao walijipitisha kwao hewani‘ una uhakika una vyumba kwa ajili yetu sote?’ yalibubujika tena maji sauti yake ikiwa haisikiki kutokana na milio na migongano ya nyangumi.

Maji hayakuweza kumsikia mwezi kwa kuwa alinong’ona kwa hofu

‘ninaamini unajaza zizi letu sana’. ‘ujinga’, jua alilalama,’ kuna vyumba kwa ajili ya kila mtu’ Lakini havikuwepo. Tayari maji yalikuwa juu ya paa, mwezi na jua walilazimika kuruka juu angani. Kuruka kwao kuliwapeleka juu sana kutoka duniani na hwakuonekana wakubwa tena. Walivyokuwa wakiruka, mwezi alimwambia jua, ‘nilikwambia alikuwa akijaza zizi letu hadi juu’. Haya yalikuwa ni maneno ya huzuni ya mwisho ambayo mwezi uliyaongea duniani.

Chanzo halisi: Nevin T (1995), Fire’s Wild Dance

Nyenzo-rejea ya 2: Dodoso kuhusu Mchana na Usiku

Nyenzo-rejea 4: Mwezi na uhusiano wake na Dunia na jua – usuli kwa ajili ya mwalimu