Nyenzo-rejea 2: Masuala ya maji

Nyenzo za mwalimu kwa kuandaa au kubadili kwa matumizi ya wanafunzi

Uchafuzi wa maji

Uchafuzi husababiswa na:

  • Takataka na mbolea za chumvuchumvi
  • Matope na mchanga (mkusanyiko wa mawe ambao huwa katika matabaka)
  • Malighafi zitokanazo na viumbe hai kama majani na nyasi zilizo katwa

Matumizi ya maji

Matumizi ya maji duniani yameongezeka mara sita zaidi kati ya mwaka

1900 na 1995 zaidi ya mara mbili ya kiwango cha ongezeko la watu-na huendelea kukua kadri kilimo viwanda na matumizi ya nyumbani yaongezekavyo. Kilimo hutumia takribani asilimia 70 ya matumizi yote ya maji duniani. Maji yatahitajika zaidi kadri watu watakavyoongezeka- inakadiriwa kuwa watu wataongezeka kutoka bilioni 6 sasa hadi bilioni8.9 ifikapo mwaka 2050

Tunaohitaji maji sio sisi tu bali kila kiumbe kinachoishi katika dunia hii pamoja nasi-na mfumi-kolojia ambapo viumbe hutegemeana

Ugonjwa

Zaidi ya watu milioni tano hufa kutokana magonjwa yatokanayo na maji kila mwaka –mara kumi ya idadi ya watu wanaokufa kutokana na vita.

Mabadiliko ya hali ya hewa

Mabadiliko ya hali ya hewa yatakuwa na athari. Baadhi ya maeneo yanaweza kufaidika na ongezeko la mvua, lakini maeneo mengine huathirika kutokana na ongezeko hilo la mvua.Tunatakiwa kufikiri tena

kwa kiwango gani tunahitaji maji kama tunajifunza namna ya kushirikiana maji. Wakati mabwawa na miradi mingine mikubwa ikiwa na umuhimu mkubwa kwa jamii duniani kuna ongezeko utambuzi wa thamani ya kutumia maji tuliyo nayo vizuri kuliko kuvuna maji bila mpangilio. Mamilioni ya watu duniani hutegemea maji ili waishi, na kukosekana kwake hupelekea kifo.

Mgawanyo wa maji duniani

Nyenzo-rejea ya 1: Kijitabu cha mimea

Nyenzo-rejea 3: Jaribio la mbegu za mahindi