Nyenzo-rejea ya 2: Maswali yanayoweza kutumika kwenye mahojiano

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Chini, ni baadhi ya maswali ya kutumia na wageni kutafiti juu ya matukio yaliyopita au namna walivyofanya vitu wakati uliopita. Maeneo unayoweza kutafiti yanajumuisha:

  • kuzalisha chakula
  • mavazi ya kale
  • tiba za asili
  • kujenga nyumba
  • Elimu

Jozi hizi tatu za masawali ya mwanzo yatakusaidia kuwapa wanafunzi msaada wa kufikiri juu ya maswali yao.

(1) matukio ya kihistoria.

  • Matukio gani ya kihistoria yalitokea wakati wa udogo wako?
  • Ulivaa nini wakati unaenda kwenye sherehe au harusi?
  • Nitukio gani unalikumbuka zaidi?
  • Unakumbuka nini juu ya hilo?
  • Nini kilitokea? Nisimulie ilivyokuwa.
  • Nani mwingine alikuwa na wewe?
  • Naweza kuongea nao juu ya hadithi hii?

(2) Michezo

  • Ni michezo gani ulicheza wakati wa utoto wako?
  • Namna gani ulicheza michezo hiyo?
  • Nani alikufundisha kucheza michezo hiyo?
  • Lini ulicheza michezo hiyo?
  • Ulichezea wapi michezo hiyo?
  • Ni shughuli gani nyingine ulizifurahia?

(3) Kuzalisha chakula

  • Mboga na matunda gani ulizalisha?
  • Namna gani ulizalisha?
  • Ulizalishia wapi?
  • Ulitumia zana gani?
  • Mboga ziligharimu kiasi gani wakati huo?
  • Ulinunua wapi? Mboga gani ulinunua?
  • Chakula gani kingine ulikula?
  • Je unaendelea kula chakula hicho?

Nyenzo-rejea ya 1: Historia simulizi

Nyenzo-rejea ya 3: Uhuru wa Tanzania