Nyenzo-rejea ya 1: Zimbabwe kuu

Taarifa za msingi/welewa wa somo wa mwalimu utangulizi

Zimbabwe kuu au nyumba ya mawe, ni jina lililotolewa kwa mamia ya ngome za mawe zilizozunguka kilomita za mraba 500 ndani ya Zimbabwe ya sasa, ambayo imeitwa kutokana na ngome hizo.

Ngome zinaweza kugawanywa katika makundi matatu tofauti yanajulikana kama Mwinuko Changamano, Bonde Changamano na eneo maarufu lililozungushiwa ukuta. Kiasi cha majengo 300 yapo katika eneo hili lililiozungushiwa ukuta. Aina za majengo ya mawe yanayopatikana katika eneo hili yanaonyesha hali ya uzalendo. Majengo mazuri zaidi yalikuwa kwa ajili ya wafalme na yalijengwa mbali na mji. Inaaminika kuwa ilifanywa hivyo kukwepa ugonjwa wa malale (ugonjwa wa kusinzia).

Mifano michache iliyopo inaonyesha kuwa Zimbabwe kuu pia ilikuwa kituo cha kibiashara, kazi za sanaa zinaonyesha kuwa mji uliunganishwa kibiashara na China. Sarafu kutoka Arabia, shanga na vitu vingine visivyo vya asili vimepatikana katika ardhi ya Zimbabwe.

Hakuna anayejua kwanini eneo hili hatimaye liliachwa. Labda ilisababishwa na ukame, magonjwa au inaweza kuwa kuanguka kwa biashara ya dhahabu iliyowalazimu watu walioishi Zimbabwe kuu kwenda sehemu nyingine. Ngome za Zimbabwe kuu ni shemu zilizochukuliwa na UNESCO tangu 1986.

Imenukuliwa kutoka: Zimbabwe Wikipedia, Website

Nyenzo-rejea ya 2: Ramani ya picha ya Zimbabwe kuu