Somo la 1

Uchunguzi wa sanaa na ughushi na jinsi vinavyotengenezwa unaweza kutoa mwanga kwa wanafunzi juu ya utamaduni wao na historia ya jamii. Pia, inakupa wewe, mwalimu, nafasi ya kubuni vizuri masomo kwa vitendo, kwa sababu kuna vitu vingi sana vya kusisimua na kazi za sanaa ambazo zinaweza kuletwa darasani kuamsha utashi, pamoja na kutoa mawazo kwa kazi za sanaa za wanafunzi.

Alama ambazo zinapatikana kwenye sanaa, mara nying zinahusiana na uadilifu na dini za jamii husika. Kwahiyo, ni muhinu kuwahimiza wanafunzi wako kuipenda sanaa-kuhifadhi urithi wao wa utamaduni na wasaidie waimaanishe katika mazingira yao. Hii ndiyo sababu tunawafundisha wanafunzi kuhusu sanaa.

Uchunguzi kifani ya 1: Kufikiria juu ya ughushi wa mahali hapo

Siku moja kabla ya somo la kwanza juu ya sanaa za asili, Bi. Kabalimu, kutoka mkoa wa Tanga Tanzania, aliwaambia wanafunzi wake watengeneze orodha ya ughushi unaotengenezwa katika jamii yao,iwe zamani au sasa. Walikuwa waongee na wazazi wao au majirani ili kupata hizi habari. Ili kuwafanya waanze kufikiria, aliwaonyesha baadhi ya mifano

ya ughushi, kama vile kikapu cha kusukwa kizuri cha Kimakonde na shanga za kuvaa shingoni za Kimasai.

Siku iliyofuata, wanafunzi waliteta orodha-Bi. Kabalimu alipitia kila moja na kuirudisha (angalia Nyenzo rejea ya muhimu 1: Kazi ya nyumbani ya kuorodhesha ughushi wa mahali hapo ). Alianza somo kwa kuwaambia wanafunzi wataje majina ya ughushi waliyojifunza, ambayo aliyaandika ubaoni. Yalikuwemo majina ya uchongaji, upakaji rangi na

michoro mbalimbali, silaha, vifaa vya nyumbani na vishirikishi. Bi. Kabalimu aliligawa darasa katika makundi madogo (angalia Nyenzo rejea ya muhimu: Kutumia makundi darasani kwako ) na kulipa kila kundi majina ya vitu viwili vya sanaa na maswali yafuatayo:

Elezea matumizi ya hivyo vitu.

Ni ujuzi gani unahitajika kutengeneza vitu hivyo? Ujuzi huu unafahamika kwa watu wengi?

Jinsi gani vitu hivi vinaweza kutunzwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya vizazi vijavyo?

Baada ya dakika 15, kila kundi liliwasilisha majibu yake kwa darasa zima. Bi. Kabalimu alitengeneza muhtasari kwenye makaratasi makubwa, na kwa kufanya hivyo, alijumuisha mawazo ya wanafunzi katika vipengele mbalimbali. Alitambua kuwa ilikuwa ni muhimu kuyajumuisha mawazo kulingana na jinsi yalivyopangwa.

Hizi karatasi zilibandikwa kwenye ubao wa matangazo wa darasa na kuachwa kwa muda wa juma moja ili wanafunzi wajifunze. Sio tu kwamba wanafunzi walikuwa wanajifunza kuhusu ughushi kwenye jamii yao, pia walikuwa wanapewa nafasi ya kujenga uwezo wa kufikiri.

Shughuli ya 1: Kuchangia mazwazo na kutengeneza sanaa za jadi na ughushi

Unaweza kuangalia katika mchoro Nyenzo rejea muhimu 2: makundi ya kuandaa aina za kazi za mikono na ughushi kukusaidia kupangilia somo hili

Kwenye majadiliano darasani, waambie wanafunzi wafikirie juu ya vitu vya sanaa asilia na ughushi wanavyovifahamu. Anza kwa kutoa mifano.

Jinsi wanafunzi wanavyotoa mawazo, yaandike ubaoni katika vipengele mbalimbali (angalia Nyenzo rejea muhimu 2).

Chunguza kila kifaa kilichosemwa kuwa ni sanaa ya uchongaji na liambie darasa lijadili ujuzi unaotakiwa ili kutengeneza hivyo vifaa, ni vipi na wapi vilitengenezwa, na ni jinsi gani vinasafishwa na kuhifadhiwa.

Fanya hivyo na kwa vipengele vingine, kwa vitu vingi kadri muda utakavyoruhusu.

Maliza somo kwa kuwaambia wanafunzi juu ya kipindi kingine cha sanaa, ambapo watachora picha au kutengeneza baadhi ya vitu. Tafuta sehemu ambapo vitu hivi vitaweza kuonyeshwa kulingana na vipengele vyake. Baadae vinaweza kuwa ni sehemu ya maonyesho ya shule.

Sehemu ya 1: Kuchunguza Kazi za Sanaa zionekanazo