Nyenzo rejea 3: Kutengenza vyungu

Taarifa za msingi/welewa wa somo wa mwalimu utangulizi

Mfano wa kutumia gurudumu la ufinyanzi

Udongo wa mfinyanzi unaweza kutengenezwa vyombo kutokana na sifa zake za pekee. Muundo wa udongo wa mfinyanzi una tabia ya ‘plastiki’ unayoufanya utengenezwe katika maumbo mbalimbali. Vifaa hivi vikiwekwa kwenye joto la kutosha vinabadilika kuwa katika hali ya mwamba mgumu, na hivyo kuwa vya kudumu. Udongo wa mfinyanzi unatokana na vitu asilia vinavyopatikana ardhini, kwa maana hiyo, unapatikana duniani kote, chini ya miguu yetu. Udongo wa mfinyazi uliwahi kutumiwa karibu na tamaduni zote, na kwa matokeo ya pekee kabisa. Vyungu vinaweza kutenengezwa kwa kutumia mikono na udongo uliochanganywa na maji.

Mfinyazi, anauandaa udongo kwa mikono yake. Vidole vinatumika kutengeneza sehemu ya chini ya chungu, halafu zinafuatia kuta katika umbo la silinda. Halafu mfinyanzi taratibu hutengeneza umbo analolitaka, kwa kutumia ncha za vidole vyake, kadiri gurudumu linavyozidi kuzunguka. Pindi kazi itakapokuwa tayari, gurudumu lililoko kwenye chungu huondolewa. Mchakato huu hurudiwa kwa ajili ya kutengeneza chungu kingine.

Wakati chungu kinapokuwa kimekauka, kinaweza kusawazishwa. Vishikio vinawekwa kwenye hatua hii. Baadhi ya aina ya mapambo yanaweza kuongezwa.

Pindi vyungu vinapokuwa vimekauka kabisa, vinaweza kuchomwa kwenye tanuru. Hii hutoa vyombo vigumu na vyepesi.

Kila chungu kinatumbukizwa moja kwa moja kwenye ndoo yenye malai kwa ajili ya kung’arishwa.

Pindi tanuru linapojaa, mlango wake unafungwa. Moto unaachwa uendelee kwa masaa 18. Vyungu vinaungua taratibu hadi joto linafikia nyuzi 1,250 °C. Katika hatua anuwai wakati moto unawaka, tanuru linaishiwa hewa ya oksijeni. Hali hii husababisha oksijeni iondolewe kwenye udongo wa mfinyanzi na ving’arisho, kitendo ambacho hupelekea mng’aro zaidi

Mfano wa kutumia mfinyo kwenye kutengeneza chungu

Kwa kuufinya udongo, unaweza kutengeneza vitu kama wanyama au bakuli, chungu, kikombe n.k. Wakati aina hii ya ufinyanzi inaonekana kuwa ya msingi, unaweza kuelewa tabia za udongo unaofanyia kazi pamoja na kujua mipaka yake (Unakunjika kirahisi? Unakauka haraka? n.k)

Kutengeneza bakuli, chungu au kikombe, anza na fundo la udongo. Kandamizia kidole gumba chako katikati, halafu finya kuta zake kwa juu.

Geuza chungu wakati unafinyanga. Hii itakusaidia kuweka unene wa kuta unaofanana.

Taratibu weka sehemu ya chini kwenye uso wa kitu ulio sawa ili kutengeneza usawa katika sehemu ya chini ya chungu.

Mfano wa chungu cha jadi – chungu cha kutunzia bangili cha Kiafrika

Chungu hiki cha jadi kuhifadhia bangili.

Imenakiliwa kutoka: Hoboken Pottery, Website and JH Pottery, Website.

Nyenzo rejea 2: Tathimini ya mawasilisho ya utafiti

Sehemu ya 3: Kutumia ngoma kujifunza