Nyenzo rejea 4: Kutafakari juu ya ngoma

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Unaweza kutumia haya maswali hapa kuwasaidia wanafunzi wako kurudi nyuma kwenye uzoefu wao. Waambie wasome na kutafakari juu ya maswali haya kwa uangalifu na kuyajibu kwa uaminifu na undani.

  1. Andika maneno matatu au zaidi kueleze jinsi ulivyojisikia wakati wa hatua zifuatazo:-
    • a.Ulivyotoa ngoma yako kwa darasa b).Kushuhudia wengine wakicheza
    • b.Kushuhudia wengine wakicheza
    • c.Kuicheza ngoma yako mbele ya hadhira
  2. Ni nini ulichofurahia zaidi juu ya masomo hayo? Kwa nini?
  3. Ni nini ulikiona kama changamoto juu ya masomo hayo? Kwa nini?
  4. Unafikiri ni jambo gani la mafanikio juu ya ngoma yako? Kwa nini?
  5. Unafikiri kuna njia za kuboresha ngoma yako? Kama ndivyo namna gani?
  6. Ni uigizaji/uchezaji gain mwingine uliopenda? Kwa nini?
  7. Umejifunza kitu chochote kipya kuhusu wewe mwenyewe?
  8. Umejifunza nini kutoka kwa michezo mingine/nyingine?

Nyenzo rejea 3: Kuboresha ngoma zetu

Sehemu ya 4: Kutumia muziki darasani