Somo la 2

Mila nyingi na imani zinaenezwa kupitia hadithi. Katika sehemu hii, tunashauri namna ya kujenga uelewa wa wanafunzi juu ya umuhimu wa hadithi katika urithisha/eneza mila hizi na kutoa ujumbe jinsi/namna watu wanavyopaswa kuishi.

Inavutia/sisimua kwa wanafunzi wasikiliza wataalamu wa hadithi akihadithia hadithi zao. Katika uchunguzi kifani 2 , mwalimu anaandaa ziara kwenda kwa mwadithiaji. Katika shughuli 2, unatumia mbinu ya kuchangia mawazo kuchunguza ufahamu wa wanafunzi wako juu ya ngano/kisa cha asili na kugundua njia za kuziweka hadithi hizi pamoja (angalia nyenzo rejea muhimu: Kutumia ramani kifani na kuchangia mawazo kugundua mawazo).

Uchunguzi kifani ya 2: Kuwapeleka wanafunzi kumtembele/kuzuru msimuliaji hadithi.

Bwana Bakari ni mwalimu wa masomo ya sayansi ya jamii na sanaa katika shule moja umasaini. Bwana Bakari alimtembelea kiongozi wake wa kijiji Mzee Sokoine, na kumuuliza iwapo awalete wanafunzi wa darasa la sita(6) nyumbani kwake. Pia alimuuliza kiongozi huyo kama atawaeleza ngano wanafunzi. Hili lilikubaliwa.

Siku moja kabla ya siku ya mapatano, ndugu Bakari aliliambia darasa kuwa atawapeleka nje ya shule kutembelea boma ya Mzee Sokoine ili wasikilize ngano za wamasai. Ili kuwaandaa wanafunzi wake, aliandaa mjadala mfupi juu ya uzoefu wao juu ya hadithi na nini wanafikiri watapata kesho yake na kuwatengenezea ramani ya kufikirika ya mawazo yao ubaoni.

Ngano/kisa alichosimulia mzee Sokoine kiko katika Nyenzo rejea 1: sauti ya kiwavi. Ngano hiyo ilikuwa na ujumbe muhimu na masomo ya kujifunza. Mwalimu Bakari, alivyosikiliza hadithi, alikuwa tayari anaandaa maswali atakayouliza darasani juu ya hadithi ili kutoa mafundisho haya. Kwa vile Mzee Sokoine alikuwa Mzee wa kuheshimiwa, aliweza kuwavutia watoto juu ya utajiri wa ukoo/jadi unaoambatishwa na hadithi za mila za kimasai ambazo zilitolewa kwa muda mrefu na maana zake ili kuziimarisha kutoka kizazi hadi kizazi nyingine. Ndugu Bakari aligundua kuwa alifanya maamuzi ya busara kwa kuwapeleka wanafunzi kwenye boma, badala ya kuwaeleza hadithi yeye mwenyewe.

Shughuli ya 2: Kutengeneza Ngano za Kiasili

Kabla ya somo, kusanya masimulizi yaliyoandkiwa na ya mdomo ya hadithi za kimila kadri utakuvyoweza. (Angalia Nyenzo rejea 2 : Hadithi na hekaya/ngano kutoka Afrika kwa ajili ya tovuti na soma Nyenzo rejea muhimu: kutumia teknolojia mpya.

Waambie

Mwanafunzi kujadiliana kuhusu ngano za asili kama ambavyo wanakumbuka kuzisikia.

Kisha, gawanya darasa lako katika makundi ya wanafunzi wanne wanne. Litake kila kundi kuchagua hadithi iliyoainishwa wakati wa kujadiliana na kuiandika kwa kirefu wakiweka wakiweka na michoro.

Toa maelekezo, kama

Jina la ngano?

Ngano hiyo inatoka jamii/ukoo gani? Ngano hiyo inatoa ujumbe gani?

Ni somo/mafundisho gani yanaweza kupatikana kwenye ngano?

Nani huhadithia hadithi?

Ni hadhira gani imelengwa na kwa nini hadhira hii imelengwa? Ni muda/wakati gani ngano husimuliwa? Kwa nini?

Ni muda gani kwa siku ngano husimuliwa? Kwa nini?

Hadithi zilizotolewa zinaweza kutenenezwa na kutumika kama vijitabu vya rejea shuleni. Inawezekana kuzichapisha na kutumika katika jamii au zaidi ya hapo.