Somo la 3

Kuwa na uelewa mzuri wa ngano za asili ni msingi mzuri kwa wanafunzi wako kubuni hadithi zao. Kusikiliza hadithi zilizohadithiwa kwa kuigizwa na kutumia maneno zinawafanya kujiamini na kuwa tayari kushiriki katika kuandika na kuzalisha/kutoa ngano zilizobuniwa vyema.

Lengo la sehemu hii ni kutumia nyenzo rejea za kawaida ili kuwajengea wanafunzi wako ujuzi wa kuandika hadithi na mashairi yao. Utaweza pia kujenga ujuzi wa kupanga shughuli za ujifunzaji unaowashirikisha wanafunzi.

Katika Uchunguzi kifani 3 mwalimu anatumia kipindi cha radio kuhamasisha wanafunzi kuhusu hadithi. Shughuli muhimu picha zinatumika kama kichocheo. Kwa watoto wadogo zaidi wanaweza kuchora picha kama hadithi zao. Ni muhimu kila mwanafunzi kuweza kutoa hadithi bila kuhangaika na kuandika maneno kwa usahii au kwa mwandiko mzuri.

Uchunguzi kifani ya 3: Kujifunza kutoka kwa mtaalam wa kuhadithia hadithi

Huku akisikiliza radio, Bi Sala, Mwalimu wa mafunzo ya jamii, alisikia kuwa Ijumaa inayofuata kutakuwa na programu/kipindi ambacho msimuliaji hadithi maarufu na mwandishi atahojiwa.

Bahati nzuri, programm/kipindi kilipangwa kwa muda mwafaka, wakati wa kawaida wa shule. Hivyo Bi Sala alikuja shuleni na radio yake. Amejiandaa pia kurekodi kipindi hicho.

Kabla ya kipindi hicho kuanza, alijadiliana na wanafunzi wake walichokijua juu ya mwandishi, na walitegemea nini kutokana na maongezi atakayotoa wakati atakapokuwa anahojiwa.

Wakati wa kipindi, mwandishi alieleza juu ya muundo wa hadithi, dhamira/wazo kuu, wahusika na mandhari. Alitoa ushauri juu ya mchakato wa unadishi. Pia alizungumzia juu ya kilichomvuta na mawazo yake aliyapata wapi. Baada ya kipindi, Bi Sala aliuliza maswali yafuatayo ili kuchochea mjadala kwa wanafunzi wake:

Unaweza kujifunza nini kutoka kwa mwandishi huyu yanayoweza kukufanya uwe mwandishi mzuri?

Kipi kinamkuchochea? Je kuna mambo katika maisha au jamii yako unayotoka kuandikia?

Uandishi mzuri/maandishi mazuri yana muundo na habari zipi? Aliuliza swali la mwisho mwishoni mwa kipindi kwa sababu alitaka

kichochewe na mambo makubwa.

Mwishoni mwa somo, alisema kuwa kwenye uandishi wa ubunifu utakaofuata, utawataka wanafunzi kujaribu mbinu zilizopendekezwa na mhadithiaji. Ataangalia ushahidi kama wamezingatia masuala haya na kwa uangalifu atatoa mrejesho.

Shughuli muhimu: Kuandika na kusimulia hadithi

Wape wanafunzi kichokoo ili kupata mawazo juu ya maisha, Jamii au Jamii pana. Angalia Nyenzo rejea 3: Picha za hadithi kwa ajili ya taswira zinazofanyakazi vizuri, lakini unaweza kuchagua kitu kingine cha kufanana/aina hiyo.

Tumia Nyenzo rejea 4: kutumia picha kama kuchokoo cha kuandika hadithi ili ikuongoze, jadili picha ambayo darasa limechagua.

Waambie wanafunzi waandike hadithi zao wenyewe. Wahamisishe kuongeze mawazo yao na matukio/ wanapoandika. Kwa mfano: Nini kilitokea kabla kilichosababisha picha itokee na nini kitafuata?

Siku inayofuata, wanafunzi walisomeane hadithi zao katika makundi madogo madogo na kila kundi linamchagua mtu mmoja wa kusomea darasa zima. Wasisitize umuhimu wa kutumia sauti na ‘vichocheo’ kama inawezekana ili viwasaidie.

Unaweza kuziweka hadithi zote kwenye vitabu vya darasa

Nyenzo-rejea ya 1: Sauti ya kiwavi