Nyenzo­rejea ya 3: Maswali ya mfano ya kuuliza kuhusu bidhaa za dukani

Nyenzo Rejea ya mwalimu kwa kupanga au kurekebisha ili kutumia na wanafunzi

  1. Ndani ya kopo/pakiti/boksi mna nini?
  2. Unajuaje hivi?
  3. Ni neno au maneno gani yameandikwa kwa herufi kubwa zaidi yaherufi zote? 
  4. Unafikiri kwa nini hili neno au haya maneno yameandikwa kwa herufi kubwa kuliko herufi zote?
  5. Maneno mangapi yanaanza kwa herufi kubwa?
  6. Maneno gani yameandikwa zaidi kwenye kifaa hiki cha kuhifadhia bidhaa kisha kuandikwa mara moja?
  7. Neno lipi hutumika sana?
  8. Nini uzito wa bidhaa hii (gramu/kilogramu)?
  9. Maneno na picha zote zinakuambia nini kuhusiana na bidhaa hii?

Maswali yanayohamasisha kufikiri kwa makini

  • Unakubaliana au unapingana na kile unachoambiwa na maneno na picha hizi?

  • Kama ungekuwa na fedha, ungependa kununua bidhaa hii? Kwa nini ndiyo?, au kwa nini hapana?

Angalizo 1: Baadhi ya bidhaa zina maneno ambayo yako kwenye lugha zaidi ya moja. Kama hivi ndivyo kwa baadhi ya bidhaa unazotumia, ungeweza kuwauliza wanafunzi ni lugha gani ambazo zimekuwa zikitumika na kwa nini wanafikiri lugha hizi zilikuwa zikitumika.

Angalizo 2: Maswali haya ya mfano ni ya jumla sana. Kuna maswali mengine mengi ungeweza kuuliza, kama kuna picha za watu kwenye bidhaa, je, ni wanaume au wanawake, je ni vijana au wazee? Kwa nini watu hawa wawepo kwenye pakiti/kopo/boksi?

Wanafunzi wanaweza kujifunza nini kutokana na kutumia orodha ya bidhaa za dukani

  1. Wasomaji wa kiwango cha mwanzo wanaweza kutumia maneno yaliyopo kwenye orodha ya bidhaa za dukani ili kupata ujasiri na stadi katika kutambua muundo wa herufi kubwa na ndogo wa alfabeti na katika kuunganisha maumbo ya herufi na sauti.
  2. Kwa kunakili herufi na maneno kutoka kwenye kitu hicho, mwandishi wa kiwango cha mwanzo, anaweza kupata ujasiri na stadi za kuandika herufi na maneno haya kwa usahihi.
  3. Wasomaji wa ngazi ya juu wangeweza kusoma ‘ujumbe’ uliopo kwenye kitu hicho na kutafakari maana yake. Wangeweza kuanza kuwa wasomaji makinifu.
  4. Kwa kufanya kazi ya kubuni baadhi ya orodha ya bidhaa za dukani katika vikundi, wanafunzi wangeweza kufaidika kutokana na mawazo ya wenzao, kujifunza vitu vinavyohusika katika kuchora bidhaa, kutumia fikra zao na kufanya mazoezi ya kuandika na kusoma.
  5. Baadhi ya wanafunzi wanaona ni vigumu kuzungumza darasani kwa sababu hawajui wazungumzie nini. Ukiwa na kielelezo cha kitu kwa ajili ya kuelezea darasani kinawapa wanafunzi mada ya kuzungumzia.
  6. Kila kielelezo cha kikundi kinawapatia wanafunzi wengine vitu vingine vya kusoma.
  7. Ungeweza kutengeneza kadi za kusomeshea zenye herufi/maneno ambayo baadhi ya wanafunzi wanayaona ni magumu kuyasoma. Weka picha ya kuwasaidia kwenye kila kadi. Tumia kadi hizi kwa ajili ya mazoezi ya kusoma ya mwanafunzi mmojammoja au kwa kikundi kidogo kwa muda muafaka.

Nyenzo­rejea ya 2: Mifano ya nyimbo na mashairi 

Nyenzo­rejea ya 4: Kujiandaa kwa matembezi ya kijumuiya – kipindi hicho wanafunzi watagundua chapa za kimazingira