Nyenzo-rejea 3: Hadithi

Nyenzo-rejea ya mwalimu kwa ajili kupanga au kurekebisha ili kutumia na wanafunzi

Andika hadithi ubaoni, lakini usiandike kichwa cha hadithi wala sentensi mbili za mwisho (‘Alitoa shuti – chini kuelekea kulia. Goli zuri!’) ubaoni mpaka sehemu ya mwisho kabisa ya somo lako.

[Kukimbilia utukufu na Mark Northcroft (umri miaka 12 )]

Alikimbia tena na tena. Miguu yake iliuma kama tindikali. Aliweza kusikia waliokuwa wanamfukuzia wakiwa wanamkaribia. Alihisi kuwa asingeweza kukaa nao sana na kwa muda mrefu lakini alijua lazima afanye vile. Hatua zilikuwa zinamkaribia. ‘Haraka! Haraka!’alilia. ‘Siwezi! Siwezi!’ alijibu. Alijisikia nguvu kutoka sehemu fulani ndani ya mwili wake. Sasa alijua kuwa atafanikiwa.

Ghafla mtu alitokea kusikojulikana. ‘Nipate sasa au nisipate kabisa,’ alifikiri.

[Alipiga shuti – chini kuelekea kulia. Goli zuri!]

Tanbihi

‘Miguu yake iliuma kama tindikali’ – Tashbiha hii au ulinganisho huu si rahisi kuueleza lakini unaweza kusema kuwa mwanaume au mvulana huyu alijisikia maumivu katika miguu yake kana kwamba kulikuwa na mchanganyiko wa kemikali iliyokuwa inachemka.

Maswali ya kuwauliza wanafunzi katika maandalizi ya uandishi wa mwanzo na mwisho mbadala wa hadithi hii

  1. Unafikiri ‘A’ ni nani?
  2. Unafikiri yuko wapi?
  3. Unafikiri nini kitamtokea?
  4. Nani ‘mwanamume’?
  5. Watu gani wengine wanaweza kuwa sehemu ya hadithi hii? 
  6. Kutakuwa kumetokea nini kabla ya sehemu hii ya hadithi?
  7. Nini kinaweza kutokea baadaye?

Nyenzo-rejea ya 2: Maswali ya kutumia wakati wa usomaji wa kitabu – usomaji wa kwanza, wa pili na wa tatu

Nyenzo-rejea 4: Usomaji kimya endelevu