Nyenzo-rejea 4: Usomaji kimya endelevu

Usuli/welewa wa somo wa mwalimu

Kukuza Usomaji Kimya Endelevu darasani kwako ni muhimu katika kuwahamasisha wanafunzi wako wapende kusoma na kuboresha stadi zao za usomaji. Ili Usomaji Kimya Endelevu ufanikiwe kunahitajika kuwe na mpango makini kabla ya usomaji wenyewe. Utahitaji kukusanya pamoja Nyenzo-rejea kwa ajili ya kusomwa na darasa au kikundi chako. Vitu hivi vinaweza kuwa makala toka magazetini, vitabu, n.k. Unatakiwa uwe mbunifu katika kukusanya vitu hivi na pia kuvihifadhi ili visipotee au visiharibike.

Kama una Nyenzo-rejea kwa darasa zima, unaweza kufanya Usomaji Kimya Endelevu mara moja kwa wiki mwanzo au mwisho wa siku. Kama una idadi ndogo ya Nyenzo-rejea, unaweza kuendesha shughuli ya usomaji kwa kutumia kikundi kimoja kwa kila siku na pia kushirikiana na darasa lako kutengeneza vitabu zaidi vya darasa vya kusoma.

Maswali ya kuuliza

Hii ni mifano ya maswali ambayo yanaweza kuulizwa kuhusu aina na viwango mbalimbali vya vitabu vya hadithi, lakini unaweza pia kuwauliza wanafunzi wakupatie maoni mafupi.

  1. Kumetokea nini katika sehemu ya kwanza (utangulizi, mwanzo) wa hadithi hii?
  2. Kumetokea nini katika sehemu ya kati (wapi pana utata au migogoro katika hadithi hii)?
  3. Kumetokea nini katika sehemu ya mwisho (suluhisho)?
  4. Je, kuna tatizo linalohitaji kutatuliwa?
  5. Nini lengo la mhusika mkuu au wahusika?
  6. Kumetokea nini kwa wahusika katika sehemu mbalimbali za hadithi? Wamekumbwa na matatizo gani?
  7. Je, umeshawahi kukutwa na jambo kama hilo?
  8. Kama jaribio lao la kwanza halikufanikiwa, je, mhusika mkuu alipata nafasi nyingine ya kujaribu kufikia lengo lake?
  9. Mwishoni kimewatokea nini wahusika?
  10. Unajisikiaje kuhusiana na hii hadithi? Je, imekufanya utafakari kuhusu maisha yako mwenyewe au ya mtu mwingine? Kama ndivyo, kwa vipi?

Kutunza rekodi ya usomaji

Wanafunzi wanapokuwa wanafanya Usomaji Kimya Endelevu ni muhimu kwao kutunza kumbukumbu ya vitabu ambavyo wameshavisoma na kutoa maoni ya kitu gani walikipenda au hawakukipenda kuhusiana na vitabu hivyo. Pia ni njia ya kujua aina ya vitu wanavyovisoma na aina ya vitu vinavyowasisimua. Utunzaji wa rekodi unakueleza wewe kuhusu wanafunzi wamesoma kwa kiasi gani, hasa ikiwa unawahimiza pia kusoma vitabu, magazeti, n.k ambavyo wanavisoma nyumbani au mahali penginepo. Kwa magazeti, unaweza kupendekeza kuwa wayaongeze kama wanayasoma mara kwa mara na waseme wameyasoma mara ngapi. Wanaweza kupendelea kuongeza makala kutoka kwenye magazeti fulani.

Kutunza kumbukumbu kusiwe kwa kuchosha kwani kutawafanya wanafunzi waache kusoma. Inatosha tu kuandika jina la kitabu na la mtunzi na labda mchapishaji kama unataka kukiweka kitabu hiki katika sehemu yake ya kukihifadhia (kama una bajeti). Wanafunzi wanaweza pia kusema kama walikipenda kitabu na kwa nini, na kama wangependekeza kisomwe na wengine.

Kumbukumbu inaweza kuwa ya darasa moja, ambapo kichwa cha kila kitabu cha maktaba kipo juu ya karatasi na kila wakati mtu anaposoma kitabu hiki anatia saini katika orodha hii na kuandika maoni mafupi. Njia nyingine ni kwa kila mwanafunzi kuwa na ukurasa mwishoni mwa daftari lake ambapo kunakuwa na orodha ya vitabu alivyosoma na kila mara anapomaliza kusoma kitabu au kusitisha kusoma kitabu anaandika maoni pembeni mwa jina la kitabu na jina la mtunzi. Itakuwa vizuri kama wanapotoa maoni waandike tarehe ili uweze kuona wanamaliza kusoma kitabu lini n.k.

Ukusanyaji na uoneshaji wa vifaa kwa ajili ya Usomaji Kimya Endelevu

Kama unahitaji kuanzisha maktaba yako mwenyewe ya darasa, hitaji la kwanza ni kukusanya vitabu na magazeti. Yapo mashirika ambayo yanaweza kuzisaidia shule kupata vitabu. Hapa kuna mawasiliano muhimu:

Mradi wa Vitabu vya Watoto Tanzania

Katibu Mtendaji

CBP

S.L.P 78245

Dar Es Salaam, Tanzania simu: (255) 22-2760750

nukushi: (255) 222-761562

baruapepe: cbp@raha.com [Tip: hold Ctrl and click a link to open it in a new tab. (Hide tip)]

Chama cha Kimataifa cha Usomaji

Makao Makuu

800 Barksdale Rd

S.L.P 8139

Newark, DE 19714-8139

Marekani

simu: +1 302-731-1600

Nukushi: +1 302-731-1057 baruapepe: pubinfo@reading.org

Huduma za Maktaba Tanzania

Mkurugenzi Mkuu

S.L.P Box 9283

Dar es Salaam

simu: (255) 22 2150048 9 baruapepe: tlsb@africaonline.co.tz

Kwa taarifa zaidi juu ya Usomaji Kimya Endelevu, wavuti hii inaweza kukusaidia:

www.trelease-on-reading.com

Wakati mwingine balozi za nchi za nje au mashirika yanayohusiana na balozi hizi, kama vile British Council, zinaweza kutoa mchango wa vitabu. Mashirika ya kutoa huduma kama vile Rotary Clubs pia hukusanya na kutoa mchango wa vitabu. Kama huwezi kuwasiliana na kampuni yoyote kwa ajili ya kuomba msaada, basi jaribu kuwaomba wenzako na rafiki zako wakupatie vitabu na magazeti ambayo watoto au wanafamilia wao wameshamaliza kazi nayo. Baadhi ya shule zinawaomba wazazi wawasaidie walimu kuendesha shughuli ya kuchangisha fedha na kisha wanazitumia fedha hizo ambazo zimechangwa kununulia vitabu. Nyenzo- rejea Muhimu: Kuwa mwalimu mbunifu katika hali zenye changamoto inatalii zaidi jambo hili.

Mara tu utakapokuwa na vitabu na magazeti ya kuwatosha wanafunzi wote darasani kwako kwa usomaji binafsi wa wanafunzi, unatakiwa utafakari namna ya kuvitunza vifaa hivi ambavyo ni vya thamani. Kama una shubaka, au unaweza kujitengenezea shubaka (au kutengenezewa na mtu mwingine), unaweza sasa kutandaza vitabu na magazeti hayo ili kuwavutia wanafunzi. Mashubaka yanaweza kupangwa pembeni au nyuma ya darasa lako. Ndani ya daftari la mazoezi andika vichwa vya habari vya vitabu na magazeti ili uendelee kuvifuatilia. Mwisho wa kipindi cha Usomaji Kimya Endelevu, kuwa makini katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wanarudisha vitabu kwenye shubaka.

Kama huna mashubaka, hifadhi vitabu na magazeti hayo kwenye maboksi. Unaweza kuwatumia baadhi ya wanafunzi kama watunzaji wa vitabu kwa kukusaidia kugawa vitabu kila kipindi cha usomaji kinapoanza na kuvihifadhi kwenye maboksi baada ya kipindi kumalizika.

Nyenzo-rejea 3: Hadithi

Sehemu ya 3: Njia za Usomaji na upokeaji wa taarifa za matini