Somo la 1

Sehemu hii inatalii njia za kufanya kazi zitakazowasaidia wanafunzi kuelezea hisia zao na kugundua mawazo yanayohusu mambo mengi, ikiwa ni pamoja na yanayohusu maisha yao. Inazingatia jinsi ya kushughulikia migongano na mikanganyiko kwa njia iliyo bora zaidi.

Mara nyingi, unapoanza mada ambazo zinagusa masuala nyeti, inasaidia kuacha wanafunzi wagundue kwa siri mawazo yao kwanza. Kwanza, kuandika mawazo kuhusu suala kunaweza kusaidia kuchochea fikira. Hii ni mbinu ambayo inaweza kutumiwa kwa mada nyinginezo ili kugundua wanachojua wanafunzi kwanza.

Uchunguzi kifani ya 1: Uandishi ili kueleza hisia na mawazo

Mwalimu Mariam Uledi wa Dar es Salaam, alijadiliana na wanafunzi wake wa darasa la 7 mambo ambayo yanawafanya wajihisi tofauti na/au kutengwa.

Baadaye, aliwataka waangalie picha ya mtoto aliyekaa peke yake wakati wenzake wakicheza ( Nyenzo-rejea 1: Mtoto ‘alitengwa’ ), na kuwataka kuandika kuhusu mtoto huyu.

Aliwauliza pia kama zamani walikwisha jihisi kama watu waliotengwa au wako tofauti na wengine au kama sasa wanajihisi hivyo. Aliwataka waandike kuhusu hisia hizo.

Halafu walicheza michezo ambayo iliwasaidia kupata ujuzi wa hali yamtu mlemavu (Angalia Nyenzo-rejea 2: Michezo inayowezesha kusaidia kuelewa ulemavu wa viungo) .

Baadaye, walizungumzia jinsi ulemavu huo unavyoweza kuwafanya watoto kujisikia tofauti na wakati mwingine kuwafanya watengwe na wenzao wa darasa. Walizungumzia juu ya watoto ambao wanaishi na virusi vya VVU/UKIMWI, au wale ambao wazazi wao wamekufa kutokana na ugonjwa wa UKIMWI. Mariamu aliwataka waandikie kuhusu ujuzi wao wakati wa michezo. Walijisikiaje kuwa na ulemavu?

Baada ya haya, kabla ya kuanza mada nyeti, mara nyingi Mariam huwataka wanafunzi wake kuandika au kuzungumza wawiliwawili au katika vikundi vidogo ili kutalii mawazo yao kwanza.

Shughuli ya 1: Kuandika ili kuibua mawazo na hisia

Wakati wa kuanza mada nyeti na wanafunzi ni vizuri kwanza kutalii mawazo na hisia zao.

Chagua picha, shairi au hadithi ili kuamsha hamasa ya kufikiri kwao. (Angalia mfano mmoja kutoka katika Nyenzo-rejea 1 ).

Waoneshe/wasome shairi au hadithi na uwatake wafikirie lina maana gani kwao.

Watake waandike au wazungumze na wenzao kuhusu mawazo yao na husisha na hisia zao pia.

Wakumbushe kuwa hakuna mtu yeyote atakayesahihisha au kuhukumu wanayoelezana. Ni kwa ajili yao kwa wakati huo kufikiri juu ya wanayofikiri na kuhisi.

Halafu, jadili pamoja na wanafunzi wanafikiri ni ujumbe upi unapatikana katika picha hizo.

Sehemu ya 4: Njia za kuwasilisha mtazamo wako