Somo la 3

Ni muhimu kujifunza namna ya kueleza hoja kwa uwazi, ukithibitisha mawazo yako. Hii ni stadi inayofaa wakati wa kuandika insha za wanafunzi, lakini pia, unapokuwa mtu mzima, kama unaandika barua kuhusu mada ya mdahalo wa kijamii au wa kitaifa hasa barua ya kuchapishwa katika gazeti.

Barua ya gazetini inaweza kulinganishwa na sehemu ya kwanza ya mdahalo.

Mara nyingi mtu mwingine atajibu barua iliyochapishwa gazetini na atatoa hoja mbadala. Katika Nyenzo-rejea 5: Mfano wa barua kuna barua katika gazeti ambayo wanafunzi wanaandika kuhusu masuala muhimu ya kuwaingiza wanafunzi wote shuleni.

Uchunguzi-kifani 3 na Shughuli muhimu inatoa mwongozo wa jinsi ya kufanya kazi na wanafunzi ili watoe hoja kwa njia ya barua.

Uchunguzi kifani ya 3: Kujifunza kuandika barua kwa mwalimu mkuu au katika gazeti

Miezi michache baada ya mwalimu Mariam Uledi kutoa wazo la kuwarudisha wanafunzi shuleni, kulikuwa na wanafunzi wageni wawili darasani kwake. Mmoja alikuwa hasikii, na mwingine alikuwa na mkono mmoja. Yeye na wanafunzi walikuwa wanaanza polepole kuwashirikisha darasani, kuzungumza nao, na kuwasaidia bila kuwafanya kujihisi kuwa wao ni ‘tofauti’ kabisa. Aliwashauri wanafunzi kuandika barua kwa mwalimu mkuu au gazetini kuhusu mada ya umuhimu wa kuwarudisha wanafunzi wote shuleni. Wangeweza kutuma barua yao kwa mwalimu mkuu au katika gazeti la Nipashe jijini Dar es Salaam, au katika gazeti la Tanzania Daima . Watapaswa kuandika kwa Kiswahili.

Wanafunzi walilipenda wazo hili na walijadiliana kuhusu watakayosema. Waliandika vidokezo vya barua.

Dhamira: Shule zijitahidi kuwarejesha shuleni ‘watoto ambao hivi sasa hawasomi.

Sababu.

‘Njia za kukabili maoni ya kupinga

Tajiriba yetu.

Kufaulu na changamoto.

Kurudia dhamira.

Mariam aliwaelekeza wanafunzi aina za virai vya kutumia, hasa namba 2 na 3, ambapo walikuwa wakiwasilisha mawazo. Walimuomba mwalimu aliyekuwa na kompyuta kuwachapia kazi yao, na kutuma nakala magazetini (Angalia barua katika Nyenzo-rejea 5 ).

Shughuli muhimu: Barua kwa mwalimu mkuu au gazetini ili kutoa hoja

Chagua mada ambayo imekwisha jadiliwa na wanafunzi katika mijadala yao na toa hoja ya kutoa mawazo yao katika barua kwa mwalimu mkuu au, kama kuna gazeti la mahali hapo, itume katika gazeti.

Uwatake wabunge bongo, katika vikundi, mambo wanayotaka kuyaandika. Baadaye andika muundo wa barua ubaoni ukitumia vidokezo vilivyomo katika Uchunguzi-kifani namba 3 (ingawa dhamira yako inaweza kuwa tofauti).

Wanafunzi wanaweza kuandika barua hii katika lugha nyingineyo (k.m. Kiingereza) hivyo wasaidie kuwapa virai vya kutumia katika utangulizi na katika hoja zao (Tazama Nyenzo-rejea 6: Virai vinavyotumika katika ‘majadiliano’ )

Vitake vikundi kutathmini barua zao na barua za watu wengine, na amua ipi ni bora ya kutuma kwa mwalimu mkuu au katika magazeti (Tazama Nyenzo-rejea 6 kwa maelekezo). Utahitaji kufanya uhariri kabla hujatuma barua, lakini jitahidi kubakiza maneno ya wanafunzi.

Fikiria wanafunzi wamejifunza nini katika kubadili majadiliano ya mdahalo hadi kwenye barua. Kwa watoto wadogo au wale wasiojiamini na wasiokuwa na uwezo wa kuandika, unaweza kulifanya kama zoezi la darasani ukiandika mawazo yao. Tumia shughuli hii kuendeleza msamiati wao katika lugha husika.

Nyenzo-rejea ya 1: Mtoto ‘aliyetengwa’