Nyenzo-rejea ya 2: Michezo inayohimiza uelewa wa ulemavu wa viungo

Nyenzo-rejea ya Mwalimu ya kutumia na wanafunzi kwa ajili ya kupanga/kurekebisha

Unaweza kuwasaidia wanafunzi kuelewa baadhi ya matatizo ambayo wanafunzi wenye ulemavu wanayapata katika kucheza michezo kama inayoelezwa hapa chini:

  1. Leta shuleni baadhi ya soksi ndefu za zamani au vipande vya kamba au sufu. Wape vifaa hivi wanafunzi na watake kuifunga mikono yao wanayoitumia kuandika nyuma ya migongo yao. Mpe kila mwanafunzi kipande cha karatasi. Waeleze kuwa mchezo huu unahusu kutaka kujua nani anaweza kuandika kwa mwandiko mzuri sentensi ambazo uko karibu kuzitaja kwa haraka. Zisome sentensi hizo na sasa angalia kutatokea nini! Baada ya kumchagua mshindi, jadiliana na wanafunzi wako walivyojisikia wakati wakicheza mchezo huu na hali ikoje kwa wanafunzi wenye ulemavu au wanaopungukiwa mkono, kama hawawezi kuandika, watake kuchora mti.
  2. Leta shuleni baadhi ya vipande vya nguo au skafu (au waambie wanafunzi kuleta vifaa hivyo) ili nusu ya wanafunzi hao waweze kufunika macho na vipande hivyo. Lichukue darasa nje. Watake wanafunzi kufanya kazi wawiliwawili. Yule ambaye amefungwa macho yake anatakiwa kutembea akipita katika vizingiti mbalimbali ulivyoweka, huku akiongozwa na mwenzake. Katika zoezi hili unaweza kutumia madawati na viti.
  3. Zingatia muda kwa kila kikundi. Kama darasa lako si kubwa sana watake wanafunzi wako wabadilishane majukumu hayo na zingatia muda tena kwa kila kikundi. Mshindi ni kikundi cha wawiliwawili waliomaliza majukumu yote kwa muda mfupi zaidi, bila kujikwaa katika kizingiti chochote. Baada ya hapo, waulize wanafunzi walijisikiaje kwa kufunikwa macho na kumtegemea mwenzao.
  4. Leta shuleni manyoya ya pamba ya kutosha kwa kila mwanafunzi ili waweze kuweka manyoya masikioni mwao ili kuwazuia kusikia vizuri. Halafu watake wanafunzi kukusikiliza wakati ukiwapa wanafunzi taarifa ya kuandika. Mshindi ni mwanafunzi wa kwanza kumaliza kuandika taarifa bila makosa. Baadaye waulize wanafunzi walijisikiaje walipokuwa hawasikii vizuri na wangefanya nini kumsaidia mwanafunzi mwenye matatizo ya kusikia.
  5. Kama shule yako inaweza, nunua pipi nyingi. Mpe za kutosha kila mwanafunzi ili midomo yao iwe imejaa pipi. Waambie wasimung’unye wala kumeza pipi yoyote bali kumwambia mwenza taarifa uliyoandika ubaoni. Hili ni gumu kulifanya na watagundua inakuwaje unapokuwa na matatizo ya kuzungumza ambayo yanamzuia mtu kusema vizuri. Mwishoni, wanakula pipi hizo!

Nyenzo-rejea ya 1: Mtoto ‘aliyetengwa’

Nyenzo-rejea ya 3: Muundo wa hotuba za mdahalo