Nyenzo-rejea ya 5: Mfano wa barua- iliyoandikwa na darasa la mwalimu Mariam

Mfano wa kazi za wanafunzi

Barua hii ni kwa ajili ya kutumwa katika gazeti, lakini unaweza kuandika barua yako kwa mwalimu mkuu kuhusu jambo jingine ukitaka.

Mhariri

Nipashe

Dar es Salaam

Ndugu

Yah.: Shule ziwalete wanafunzi wanaokaa majumbani

Katika Tanzania, elimu ya msingi ni bure. Ni kwa ajili ya watoto wote. Lakini bado kuna watoto ambao wamekaa majumbani, bila kusoma. Baadhi wana ulemavu, wengine wana wazazi wao wenye virusi vya UKIMWI, na wazazi wengine ni masikini mno kiasi cha kutoweza kuwanunulia watoto wao sare za shule.

Shule lazima ziwalete watoto hawa mashuleni, ili wapate elimu na wenzao. Kwa nini tunasema hivyo?

Kwanza, ni haki yao ya kidemokrasia kuelimishwa. Waziri wa elimu anasema kuwa watoto wote lazima wajumuishwe darasani.

Pili na muhimu zaidi, wahitaji kuwa na marafiki na kuwa sehemu ya maisha.

Baadhi wanasema kuwa walimu hawajui kuwafundisha wanafunzi wenye ulemavu. Wengine wanasema kuwa wazazi hawataki watoto wao kuwa na marafiki ‘walemavu’ Lakini hatutaki jumuiya yetu iwe ile ya kubagua. Kila mmoja lazima ashughulikiwe kwa namna ileile.

Watoto wanaweza kuwasaidia wenye ulemavu, na kulifanya kuwa jambo jepesi kwa mwalimu.

Darasa la saba katika shule ya msingi Bunge jijini Dar es Salaam iliwakuta watoto wawili wakiwa peke yao nyumbani. Tuliwahimiza kuja shuleni. Kibena alikuwa na mkono mmoja. Tunamsaidia kujifunza kuandika na kucheza michezo. Ni hodari na anajifunza kwa haraka.

Masanja ni mlemavu asiyesikia, lakini akikuangalia midomo yako, anaweza kusikia. Anajitahidi. Pia amekuwa hodari wa kusoma. Tunaweza kumuandikia ujumbe. Tunajifunza mambo mengi kutoka kwa watoto hawa, na marafiki zetu.

Bado ni vigumu kwao, na mwalimu anawapa msaada wa ziada baada ya shule. Kamati ya shule inawasaidia pia kwa kuwanunulia sare za shule. Bado hawana sare za shule.

Tunafurahi kuwa wamekuja darasani mwetu, na tunataka kuziambia shule nyingine kufanya kama tulivyofanya sisi.

Wako

Darasa la 7, Shule ya msingi Bunge

Nyenzo-rejea ya 4: Sheria na taratibu za kuendesha mdahalo

Nyenzo-rejea ya 6: Vifungu vya utoaji hoja