Somo la 1

Sote husimulia hadithi, kuhusu maisha yetu ya kila siku au yaliyopita.We all tell stories, about our daily lives or about the past. Kuna desturi nyingi katika usimuliaji hadithi na mafundisho mengi kutoka kwenye hadithi. Shughuli 1 talii kutafiti ni nini, unafanywaje, na matokeo yanaweza kuchanganuliwa. As you work alongside the class on the task, utajifunza ni nini wanafunzi wako wanakiweza.

Tunashauri usome Nyenzo-rejea muhimu: Kuchunguza darasani kabla ya kuanza. Kama ungependa kusoma tafiti za watu wengine, Nyenzo-rejea 1: Ngano za kimapokeo pia ni nzuri, inatoa taarifa juu ya warsha iliyofanyika Qunu mashariki ya rasi ya Afrika-kusini, ambapo wazazi, walimu na wanafunzi walijadili maswali unayotafiti.

Uchunguzi kifani ya 1: Kutafiti ni kwa nini watu husimulia hadithi

Bibi Rashe na wanafunzi wake wa darasa la 3 katika shule ya Nqamakwe, mashariki mwa rasi ya Afrika kusini husimulia hadithi kila siku.

Siku moja aliandika swali ubaoni ‘Kwa nini watu husimulia hadithi?’ na kuorodhesha majibu ya wanafunzi:

Kufurahisha

Kuogopesha watu

Kunifundisha nisifanye jambo fulani.

Alimuomba kila mwanafunzi aende nyumbani na kumuuliza mtu mzima swali hilo hilo na kuleta majibu. Alihakikisha kwamba amewakumbusha wanafunzi kuwa wanatakiwa kuwakabili watu kwa unyenyekevu pindi wanapouliza maswali. Pia aliwakumbusha kuelezea vipi taarifa zingetumika.

Siku iliyofuata aliongezea majibu yao kwenye orodha. Pale ambapo watu zaidi ya mmoja walitoa jibu sawa aliongeza alama (√) (angalia Nyenzo-rejea 2: Kwa nini watu husimulia hadithi ).

Aliwaomba wanafunzi kuongeza tiki kwa kila sababu. Walijadili maswali yafuatayo:

Sababu zipi ni maarufu sana? Umejuaje? Unakubaliana na mawazo ya wakubwa? Kwa nini ndio/hapana? Baada ya majadiliano, Bibi Rashe aliwaomba wanafunzi wake waandike wamepata nini kutokana na utafiti wao.Siku iliyofuata, aliwaomba wanafunzi wachahe wenye mawazo tofauti kusoma ripoti zao. Alikuwa akishangazwa na kufurahishwa na mawazo tofauti ambayo wanafunzi walikuja nayo.

Shughuli ya 1: Kuchunguza usimuliaji hadithi

Waeleze wanafunzi kuhusu utafiti, tumia Nyenzo-rejea muhimu: Kuchunguza darasaniikusaidie kupanga unachotaka kusema. Waeleze kuwa watakusaidia katika kuchunguza usimuliaji wa hadithi (angali Nyenzo-rejea muhimu: Kuelezea na kuonesha darasani)

Andika maswali ubaoni kutoka katika Nyenzo-rejea 3: Maswali kuhusu hadithi .

Eleza kuwa kila mwanafunzi ataenda kuuliza maswali haya kwa mtu mzima mmoja miongoni mwa jamii. Wakumbushe pia kuwakabili watu wazima kwa heshima na kurekodi majibu watakayopewa.

Siku kadhaa baadaye, wagawe wanafunzi katika makundi ya watu sita mpaka nane na waache waorodheshe (kwa kila swali) majibu waliyoyapata; ongeza alama ya tiki kwa jibu lililotolewa na mtu zaidi ya mmoja.

Sasa kila kundi liripoti, na wewe kumalizia seti ya data (taarifa zilizokusanywa na darasa) ubaoni.

Jadili mawzo yaliozoeleka sana. Je, wanafunzi wanakubaliana nayo?

Wasaidie wanafunzi kuandika ripoti rahisi kuhusiana na walichokipata (angalia Nyenzo-rejea 2 kwa mpango wa ripoti ya utafiti).

Sehemu ya 1: Kuchunguza hadithi