Somo la 2

Unapokuwa na matokeo ya utafiti, yanatakiwa yatafsiriwe ili uweze kutumia taarifa. Katika mfano wetu, hii ina maana kuwasaidia wanafunzi wako kutumia taarifa iliyopatikana kuelewa hadithi zaidi. Shughuli 2 inakusaidia kutalii maana katika hadithi kama ufuatiliaji baada ya uchunguzi.

Uchunguzi-kifani 2 inatambulisha wazo muhimu la kuwasaidia wanafunzi kutunga maswali yao wenyewe na kujaribu kuyatafutia majibu. Kuweza kuuliza maswali yao wenyewe katika makundi madogo huwajengea fikra huru na hukuza uwezo wa wanafunzi wa kufikiri kiubunifu na kwa makini.

Uchunguzi kifani ya 2: Kumalizia hadithi

Bibi Mwenda kutoka Dodoma alifanya utafiti makini katika vipengele vya hadithi nzuri ambayo haifahamiki sana (angalia Nyenzo-rejea 4: Namna Bibi Mwenda alivyopata hadithi yake ).

Siku moja aliwakusanya wanafunzi wake wa darasa la 2 kumzunguka, na aliwasimulia sehemu ya kwanza ya hadithi (aya tatu za mwanzo za Nyenzo-rejea 5: Mto ambao ulifagilia mbali waongo ). Baadaye, aliwaomba kila mmoja afikirie swali juu ya kingetokea nini katika sehemu iliyobaki ya hadithi. Baada ya dakika mbili walimpa maswali yao, na aliyaandika ubaoni.

Aliomba darasa kufikiria majibu ya maswali, kuchukua swali baada ya swali. Wanafunzi walitoa sababu za majibu yao.

Baada ya kuyapitia maswali na majibu yote, aliwaomba kumsaidia kuandika mwisho wa hadithi. Wallipendekeza nini kingeweza kutokea baadaye na aliyaandika maoni yao ubaoni. Hakukurupua mchakato, au kulazimisha mawazo yake kwa wanafunzi.

Pale hadithi ilipokuwa imekamilika, waliisoma kwa pamoja.

Wanafunzi walipenda kushughulika pamoja kwenye hadithi. Siku iliyofuata, katika watu wawili wawili, walichora picha za sehemu mbalimbali za hadithi. Hizi ziliwekwa pamoja katika kitabu.

Mwisho, Bibi Mwenda aliwasomea hadithi yenyewe. Wanafunzi walifurahishwa na mwisho wa hadithi zao ikilinganishwa na mwisho wa hadithi halisi na walizungumza mengi juu ya matatizo ya kusema uongo.

Shughuli ya 2: Kujadili kwa nini hadithi maalumu husimuliwa

Chagua hadithi nzuri kutokana na unazozijua. Hakikisha una masimulizi kamili ya hadithi.

Andaa nakala moja kwa kila kikundi katika darasa lako, au uandike hadithi ubaoni, mahali ambapo wanaweza kuiona wote.

Pia andika sababu za kusimulia hadithi zilizotokana na utafiti wa darasa.

Wambie wanafunzi wako kujadili katika makundi kwanini wanafikiri watu wangewasimulia hii hadithi (k.v lengo lake).

Kadri makundi yatoavyo ripoti, waambie waeleze sababu zao. Kasha, jadili wahusika wa hadithi na tabia zao.

Waulize wanafunzi ni jinsi gain wangeweza kutumia hadithi hii katika maisha yao wenyewe.

Waambie, katika makundi, kujadili lengo la hadithi nyingine, labda moja kutoka nyumbani na kasha kuandika aya juu ya lengo la hadithi.

Je, wote walielewa malengo ya hadithi zao? Umelijuaje hili?

Hii shughuli haihitaji kumalizwa kwa muda wa somo wa dakika 30. inaweza ikaendelea katika vipindi vya somo jingine kama wanafunzi wako wana mambo mengi ya kujadili.