Somo la 3

Utafiti unaonesha kuwa watu hujifunza vizuri pale ambapo kile kilichokuwa kikifundishwa ni muhimu kwao. Ukiwa kama mwalimu daima unatakiwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wako wanapata maarifa ambayo yatawasaidia kuuelewa ulimwengu wao.

Wewe na darasa lako mmetafiti ni kwa nini watu husimulia hadithi na mmeangalia maana ya hadithi maalum. Sasa tunaangalia ni jinsi gain unaweza kuwasaidia wanafunzi wako kutumia usimuliaji wa hadithi katika hali ya maisha halisi na kwenye matatizo.

Uchunguzi kifani ya 3: Kuandika hadithi

Bibi Kaniki alitaka kuwasidia wanafunzi wake wa darasa la 6 pale Arusha kuandika hadithi zao wenyewe katika vikundi vya watu wawili wawili. Aliandika orodha ya sifa yamkini za hadithi (angalia chini) ubaoni na alizijadili na wanafunzi wake jinsi sifa hizo zinaweza kuabiri aina ya hadithi inaandikwa.

Wanyama wanawakilisha binadamu

Matukio ya ajabu, viumbe visivyo vya kawaida

Mtu kupata matatizo na kutafuta njia ya kuyatatua

Mwema na muovu

Maelezo ya jinsi vitu vilivyo

Pia aliwapa orodha ya matukio, mazuri na mabaya, yaliyotokea mjini hivi karibuni na alipendekeza watumie moja ya matukio haya kama muktadha wa hadithi zao. Baadaye , aliwaambia wachague ikiwa wahusika wa hadithi zao wangekuwa ni watu au wanyama. Mwisho, aliwauliza dhamira wangechagua, kama vile vita kati ya wema na uovu. Walipokuwa wamshaamua dhamira, aliwapa moyo kila kikundi cha watu wali kuanza kuandika.

Baada ya wiki moja au mbili, Bibi Kaniki aliliambia kila kikundi kuchangia (mawazo) ya hadithi na darasa zima, halafu walijadili lengo la hadithi lilikuwa lipi. Aliridhishwa na aina anuai za hadithi.

Shughuli muhimu: Kutunga hadithi mpya (halisi)

Waambie wanafunzi wafikirie matatizo katika familia zao, shule na jamii ambayo hutokana na jinsi wanavyotendeana. Matatizo yangeweza kuanzia yale ya kila siku, kama uvivu hadi mambo mazito, kama vile virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Ungeweza kuwachochea kwa kueleza hali za kawaida zinazohusisha baadhi ya aina za tabia, lakini kuwa makini na hali binafsi za wanafunzi katika darasa lako. Ungeweza kutumia magazeti kusaidia kupata mawazo ya hadithi.

Kila kundi lichague tatizo moja na kulitungia hadithi ambayo inaonesha athari za aina hii ya tabia na kutoa busara juu ya tabia hiyo.

Jadili baadhi ya sifa za hadithi kabla hawajaandika hadthi zao au panga jinsi gain wataisimulia (angalia Uchunguzi-kifani 3 ).

Waambie kila kundi kusimulia hadithi zao darasani. Jadili lengo la kila hadithi, yaorodheshe, na yalinganishe na matokeo ya utafiti wao kutoka Shughuli 1.

Waache wanavikundi wajiamulie kama hadithi yao ilifanikiwa na kwa nini (Angalia maswali katika Nyenzo-rejea 6: Kuikadiria hadithi yako .)

Kwa kiasi gani walifanikiwa kujikadiria?

Je, unakubaliana na makadirio yao?

Kama una wanafunzi wadogo, ungeweza kufanya zoezi hili kama shughuli ya darasa zima ambapo unaandika mawzo yao ubaoni au kwenye karatasi.

Nyenzo-rejea ya 1: Ngano za kimapokeo