Nyenzo-rejea ya 1: Ngano za kimapokeo

Usuli/taarifa ya mwanzo/uelewa wa mwalimu

Usuli

Warsha iliendeshwa kama sehemu ya kazi za kitengo cha maendeleo na kisomo vijijini cha mfuko wa Nelson Mandela na shule tano kutoka eneo la Qunu mashariki mwa rasi zilishiriki. Kutoka kila shule kulikuwa na walimu wawili na mwanafunzi mmoja na mzazi mmoja na mjumbe mmoja wa kamati ya shule.

Lengo la warsha lilikuwa ni kuakisi pamoja juu ya thamani ya ngano za kimapokeo katika elimu ya watoto na jamii, na kupanga njia za kutumia hadithi hizi ndani na nje ya shule.

Kifuatacho ni ripoti ya majadala uliokuwa ukiendeshwa katika makundi katika siku ya kwanza ya warsha. Washiriki walitoa mawazo yao.

Je, unakubaliana na mwazo na maoni yao?

Ngano ni nini?

Ngano ni hadithi fupi zenye lengo maalum, zina baadhi ya mafundisho, ucheshi, maonyo. Husifu, hukosoa na hurekebisha. Hunoa ubongo kuufanya ufikiri kwa makini na hujenga ufikiriaji wa kina. Baadhi ni matukio halisi ambayo baadaye hubadilishwa kuwa ngano; baadhi zimekuwa zikitungwa maalum kwa dhamira ya kuchoma au kuumiza ili kuachana na matukio yaliopita na kufundisha staha.

Ni watu gain husimulia au husimuliwa ngano?

Kwa kauli moja walisema ni watu wazima- bibi na babu, pia watoto wenyewe kwa wenyewe, kipindi cha mafunzo ya jando na unyago. Pia walimu, watangazaji wa redio na luninga husimulia hadithi.

Waliwasimulia/huwasimulia nani?

Zilisimuliwa kwa watoto, vijana na watu wazima.

Lini na wapi ngano zinasimuliwa/zilisimuliwa?

Chumba cha kupumzikia mara nyingi hutumika, wakati mwingine chumba cha kulala na mara nyingine hadithi zilisimuliwa wakati wakiota jua karibu na maboma ya ng’ombe. Seheme nyingine zilikuwa kingo za mito, malishoni, viwanja vya nyumba na kwenye kumbi za jando na unyago.

Kwa nini walisimuliwa/ wanasimuliwa hadithi?

Zilikuwa kwa ajili ya kufurahisha, kunoa ubongo, kama kikumbushi, kama katazo au onyo, kuchochea uzalendo kupitia tabia fulani, kutupa msamiati na vitatanishi vyake (kama tamathali za usemi, nahau, methali na maneno mapya ambayo huingia kwenye kamusi).

Wanasimuliwaje/ walisimuliwaje hadithi? (mtindo wa usimulizi)

Kulikuwa na mashindano katika usimuliaji wa hadithi. Ilikuwa sanaa, iliyohusisha muziki, ucheshi na kubadili sauti. Ngano za kimapokeo zina mwanzo na mwisho wa pekee.

Hadithi mpya husimuliwa kama zinavyosimuliwa hadithi za zamani? Kwa sababu zipi hadithi mpya hutungwa ?

Ngano za zamani na mpya zimekuwa zikitumika, na hufanya kazi moja.

Kwa kawida, hadithi mpya hujumuisha maeneo yote mpya za maisha.

Je, una masimulizi ya ngano yalioandikwa? Yataje.

Kuna ngano za zamani chache zilizo katika maandishi ( Baadhi zimetajwa)

Kilichokuwa kimeonekana ni kwamba ngano chache sana zilikumbukwa na kundi na haikuwa kazi rahisi kufanya hivyo.Mtu mmoja pekee alikumbuka tatu, baadhi hawakuweza kukumbuka yoyote. Kutokana na washiriki 23, ngano 19 tu zilitolewa. Hii inamaanisha nini?

Wapi na kwa namna gain ngano zilizoandikwa hutumika?

Ngano husomwa kutoka vitabuni mara kwa mara. Ndicho kinachotokea nyumbani ambapo ngano zile zile hurudiwa kusimuliwa kwa kujifurahisha. Shuleni husomewa watoto. Zina mchango kwa msamiati wa watoto. Ni chache. Kuna baadhi katika maktaba na wakati mwingine huigizwa jukwaani.

Lugha inayotumika

Lugha iliyozoeleka ni lahaja, lugha za kitoto pia hutumika, vile vile maneno yalioundwa kuonesha staha

Dondoo limendondolewa kutoka ripoti ya warsha juu ya ngano za kimapokeo iliyofanyika Qunu, Rasi ya Mashiriki.

Nyenzo-rejea ya 2: Kwa nini watu husimulia hadithi