Nyenzo-rejea ya 2: Kwa nini watu husimulia hadithi

Mfano wa kazi za wanafunzi

Ubao wa Bibi Rashe

Ni kwa nini watu husimulia hadithi?

kufurahisha √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ 35

kuogopesha watu √√√√√ √√ 7

kunifundisha kutofanya jambo fulani √√√√√ √√√√√ 10

kufundisha busara juu ya maisha √√√√√ √√√√√ √√√√ 14

kuonesha tabia sahihi, √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√√√√ √√ 32

kukuza lugha yetu, √√√√√ √√ 7

mpango wa ripoti ya utafiti

Swali la utafiti

Tulifanya nini

Tunachambuaje data

Tulipata nini

Ripoti juu utafiti wa hadithi

Wanafunzi wa darasa la 3 waliwauliza watu wazima: ‘Kwa nini watu husimulia hadithi?’

Watu wazima wapatao 35 walilijibu swali hilo.

Wanafunzi waliandaa orodha ya majibu, na walihesabu watu wangapi walijibu kila swali.

Kifani cha ripoti

Watu 34 walidhani kuwa hadithi husimuliwa kwa ajili ya kuwafurahisha wasikilizaji.

Watu 32 walidhani kuwa hadithi husimuliwa ili kuonesha tabia nzuri/sahihi.

Watu 14 walidhani kuwa hadithi husimuliwa ili kufundisha busara katika maisha.

Watu 10 walidhani kuwa hadithi husimuliwa ili kufundisha watu kutofanya jambo fulani.

Watu 7 wao walidhani hadithi husimuliwa ili kukuza lugha.

Watu 7 walidhani kuwa hadithim husimuliwa ili kuogofya watu.

Nyenzo-rejea ya 1: Ngano za kimapokeo

Nyenzo-rejea ya 3: Maswali kuhusu hadithi