Nyenzo-rejea ya 4: Namna Bibi Mwenda alivyopata hadithi yake

Usuli/taarifa ya mwanzo/uelewa wa mwalimu

Patricia Mwenda alijaribu kutafakari juu ya hadithi ambayo haikutambulika sana. Aliikumbuka nahau iliyorandana na hadithi yake. Nahau yenyewe ilisema: ‘Hakuna mbweha aliye mkubwa kuliko mwingine, mbweha wote wana umbo sawa.’ Alikumbuka kuwa hadithi ilikuwa juu ya Bwana na mtumishi wake waliokuwa wakisafiri juu ya farasi, na yule mtumishi alimsimulia Bwana wake juu ya hadithi ya mbweha aliyekuwa na umbo la ndama au maksai. Bibi Mwenda alikumbuka pia kulikuwa na mito ipitayo, na mmoja wapo uliitwa ‘mto unao somba waongo wote’. 

Alipokuwa hana uhakika na nini haswa kilijiri, alimuuliza wifi yake aitwaye Amina juu ya hadithi. Amina alimwambia kuwa, mtumishi yule alikuwa muongo sana. Hapo zamani alijaribu pia kusimulia hadithi ya kunguni kumfananisha na kitu kikubwa sana, hadithi ambayo haiwezi kuwa kweli. Bado walikuwa na tondoti chache, hivyo walikwenda kwa Bwana Majengo ambaye aliyewahi kuwa mwalimu wa Kiswahili, kwa sasa ni mkaguzi wa shule. Hakuweza kukumbuka hadithi, lakini alikumbuka kuwa tafsiri yake ipo kwa msomaji maalum.

Siku moja, Patricia alikuwa akiongea na Bi. Kolisa Ngodwana, mwalimu wa hisabati, aligundua kuwa alifamu ujumbe uliopo kwenye hadithi. Alisema kwamba yule Bwana alitumia mbinu fulani kumsimamisha yule mtumishi kudanganya. Hakutaka kumshutumu moja kwa moja kwa uongo. Bi. Ngodwana alisema kuwa mbinu zile zilifanikiwa, kwani mtumishi alitubu na kuzungumza kabla ya kufika mtoni. Lakini Bw. Ngodwana pia hakuweza kukumbuka tondoti za hadithi yote.

Kisha Patricia alikwenda kwa Bw. Mr Hintsa Siwisa, mwanasheria. Alijua nahau na ujumbe wa hadithi. Alifikiri ilitokana na jamii kuchoshwa na uongo wa mtu yule. Waliamua kumuweka kwenye jaribio la nguvu na kumpa somo. Masimulizi ya hadithi ya Bw. Siwisa ipo kwenye Nyenzo- rejea 5: Mto uliofyagilia mbali wa waongo.

Imenakiliwa kutoka: Umthamo 2, University of Fort Hare Distance Education Project

Nyenzo-rejea ya 3: Maswali kuhusu hadithi

Nyenzo-rejea 5: Mto uliofagilia mbali waongo