Nyenzo-rejea 5: Mto uliofagilia mbali waongo

Nyenzo ya mwalimu kwa ajili ya mpango au utohozi utakaotumiwa na wanafunzi

Bwana mmoja alikuwa safarini na mtumishi wake. Ilikuwa ni safari ndefu juu ya farasi. Kadri walivyokuwa wakisafiri, yule Bwana aliona mbweha akikatiza kwenye njia.Yule Bwana alisema: ‘Mbweha yule ni mkubwa sana.’ Yule mtumishi akajibu, ‘Oh, Bwana huyu si chochote ukilinganisha na niliyemuona jana.’ ‘Ndivyo hivyo?’ alidakia yule Bwana. ‘Oh! Ndiyo, Alikuwa mkubwa sana sana. Kwa hakika alikuwa mkubwa kama maksai!’ ‘Mkubwa kama maksai?’ Bwana aliuliza. ‘Ndiyo mkubwa kama maksai,’ alijibu mtumishi. Bwana akasema tena, ‘Umesema “ni mkubwa kama maksai”?’ ‘Ndiyo haswa, mkubwa kama maksai,’ alisema mtumishi. Yule Bwana hakusema neno waliendelea na safari yao, bila kusemezana takribani kwa muda wa saa moja.

Mtumishi alibaini kuwa Bwana wake hakuwa na raha na hukujua ni nini kilimsumbua. Kwa hiyo alimuuliza alikuwa na jambo gani. Yule bwana alimwambia kwamba wangevuka mito minne kabla ya kufika mwisho wa safari yao. Mto wa mwisho ni mkubwa na hatari zaidi kuliko yote. Mto huu ulikuwa na mzio na waongo na hakuna mwongo angeweza kuepuka hasira yake. Iliwazoa waongo huku na huko hadi kwenye kina kirefu cha bahari ya bluu. Haikuwahi kumkosa mwongo hata kama wakimuomba ‘Ifa’ awaletee bahati (watu humuomba Ifa awaletee bahati, na kuwapa nguvu ya kuwashinda pepo waovu).

Mtumishi aliposika hivi, alitishika sana kwa sababu alijua uwezo aliokuwa nao Ifa. Kama mto huu usingeshindwa na Ifa, basi alijua wazi kuwa ni lazima utakuwa ni mto wenye nguvu SANA. Kwa kadri walivyokuwa wakiendelea na safari ndivyo alivyoendelea kukosa utulivu. Bwana wake naye aliendelea kukasirika sana. Na jinsi anavyoendelea kukasirika ndivyo mtumishi wake alivyoendelea kushikwa na hofu na hofu kubwa.

Wakati walipokwa wanaukaribia mto mmoja baada mwingine, ndivyo umbo la mbweha nalo lilivyokuwa likipungua. Walipoukaribia mto wa kwanza, mtumishi alisema, ‘Bwana wangu, mbweha si mkubwa kabisa kama maksai, ni mdogo kidogo kuliko maksai.’ Bwana hakusema kitu chochote.

Walipoufikia mto wa pili, mtumishi alisema , ‘Mbweha hata hakaribiani kwa umbo na maksai. Ni mkubwa kama ndama.’ Lakini yule Bwana, akaendelea kukaa kimya. Walipovuka mto wa pili yule Bwana alieleza jinsi anavyojisikia kuhusiana na ule mto hatari wa mwisho na hakusema kitu tena.

Walivyoukaribia mto wa tatu, mtumishi alimwambia Bwana wake, ‘Mbweha sio mkubwa kama ndama. Ni mkubwa kama mbuzi.’

Kabla tu hawajakaribia mto wa mwisho, mbweha alikuwa na umbo sawa na mbweha wengine, ambao hupatikana kila sehemu.

Imenakiliwa kutoka: Umthamo 2, University of Fort Hare Distance Education Project

Nyenzo-rejea ya 4: Namna Bibi Mwenda alivyopata hadithi yake

Nyenzo-rejea 6: Kukadiria hadithi yako