Somo la 2

Kuwaalika wanajumuia darasani kutasaidia katika kuwahamasisha wanafunzi na kuwajengea ustadi katika kusimulia hadithi kwa kutumia lugha zao za asili. Unaweza pia ukawataka wageni wako kutumia ujuzi wao wa hadithi ili kuhakikisha kwamba hadithi zinazosimuliwa na wanafunzi ni za kweli na zenye kujitosheleza kadiri iwezekanavyo. Hii itamaanisha kwamba hadithi zitakuwa nyenzo za msingi ya kujifunzia.

Kama una darasa kubwa, aina hii ya uungwaji mkono na jumuia inasaidia sa Kuomba kuungwa mkono na mkuu wako wa shule na walimu wenzio kutalifanya jambo hili kuwa katika msingi unaoeleweka.

Uchunguzi kifani ya 2: Kuwaalika wanajumuia katika siku wanajumuiya

Walimu wanne wa shule ya msingi ya Mtakatifu Maria iliyopo Dar es Salaam wameandikishwa katika programu ya kuwaendeleza walimu. Moja ya moduli katika programu hii, inawataka kuchunguza ni kwa namna gani Nyenzo-rejea zinazowazunguka zinaweza kutumika darasani. Walifanya kazi ya kukusanya maboksi, chupa, mimea na nyenzo nyingine na kuzitumia katika mazoezi ya sayansi, hesabu na lugha.Hata hivyo, moduli ziliwakumbusha kuwa watu ni nzenzo muhimu kwa ajili ya kujifunzia.

Ilipendekezwa kuwa wapange siku ya kuwakutanisha pamoja wanafunzi na wanajumuia wanye umri mkubwa kwa lengo la kubadilishana maarifa na ujuzi.

Siku ambayo walimu hawa wanne waliipanga, ilikuwa na mafanikio makubwa. Bibi Rwakatare, mwenyekiti anayeongoza bodi ya shule, alielezea historia ya shule. Baadhi ya wanajumuia walioshiriki walionesha kwa vitendo stadi mbalimbali kama vile,ususi wa vikapu,ukaushaji wa tumbaku, na kutengeneza shanga,.wanawake walisifika kwa kutoa maelezo kuhusu mapishi ya vyakula vya asili. Wazee mbalimbali, wanaume kwa wanawake walisimulia ngano.

Kisha ikafuata zamu ya wanafunzi kuonesha kwa vitendo mambo waliyojifunza shuleni. Siku ilimalizika kwa kuimbwa nyimbo na dansi toka katika vikundi mbalimbali.

Kutokana na shughuli za siku hii, wanajumuia mbalimbali wakawa wanatembelea shule mara kwa mara. Walitoa ujuzi wao katika stadi mbalimbali na pia walisimulia hadithi ambazo baadaye zilitumiwa darasani.

Shughuli ya 2: Mafunzo toka wanajumuia ‘mahiri’

Utatakiwa kupangilia vema shughuli hii mapema na kutenga muda wote wa asubuhi au mchana kwa ajili ya shughuli hii.

Wapange wanafunzi wako katika vikundi kulingana na lugha zao za nyumbani. Waagize kila kikundi kualika mtu mmoja toka katika jumuia zao kuja darasani ili kuwasaidia wanafunzi katika ustadi wao wa kusimulia hadithi. Wape kila kikundi barua ya mwaliko waendenayo nyumbani. (tazama Nyenzo-rejea 1: Mfano wa barua ya mwaliko ).

Waagize wanajumuia wajiunge na kikundi na kusikiliza wanafunzi wakiwa wanasimulia hadithi siku hiyo. Waombe wageni waalikwa wawape wanafunzi muongozo na ushauri juu ya namna ya kuboresha hadithi na masimulizi yao.

Kipindi cha mafunzo kikimalizika, vikundi vinaweza kukaa pamoja na kusikiliza hadithi kutoka kwa wageni waliowaalika. Nyimbo, mashairi na vitendawili vinaweza vikatolewa siku hiyo.

Je, ushirikishwaji wa wanajumuia umeongeza nini katika ujifunzaji darasani mwako?

Je umefurahia namna ulivyopangilia shughuli zako?

Je utafanya nini cha tofauti wakati ujao?