Somo la 3

Ni muhimu kila mwanafunzi awe na uwezo wa kuwasiliana vema na kuwa kuwa anapewa nafasi ya kuwa mbunifu.Uwasilishaji wa hadithi katika vikundi unatoa nafasi hata kwa wanafunzi wakimya kuzungumza, kuimba, kutenda,kucheza n.k bila ya shinikizo. Kila mwanafunzi katika uigizaji wa hadithi anaweza kupata nafasi ya kuwa muhusika katika hadithi, msimuliaji ama kuwa sehemu ya kiitio. Wanafunzi wenye vipaji maalum wanaweza wakaandaa ‘vifaa’ na ‘mavazi’ wakiwa na vitu kama vipande vya nguo ama karatasi ama matawi ya mti.

Katika madarasa ambapo wanafunzi wote hawazungumzi lugha moja ya nyumbani, kufanya kazi na wazungumzaji wa lugha inayofanana kwa lengo la kuandaa uigizaji katika lugha hii kunaweza kuwa na matokeo bora.

Sehemu inayofuata inakupa njia ya kukuza kujiamini na stadi kwa wanafunzi katika lugha zao za nyumbani. Njia hizi pia zinaweza zikatumika katika kuimarisha stadi katika lugha ya mawasiliano ama lugha ya ziada.

Uchunguzi kifani ya 3: Siku ya kuigiza hadithi katika darasa kubwa

Bibi Rebecca Kassam hufundisha darasa la tano lenye wanafunzi 100, katika kijiji kilichopo karibu na Tanga Kaskazini mwa Tanzania. Aliamua kuwa na siku ya kuigiza hadithi mwisho wa muhula. Aliwapanga wanafunzi wake katika vikundi vya watu watanowatano na kisha kuwahimiza sio tu wasimulie hadithi bali pia waigize, hivyo, waigizaji na hadhira kwa pamoja wataweza kufurahia. Aliwaeleza wanafunzi kwamba kama watataka kuigiza katika lugha ambayo si kila mtu anaifahamu, hawana budi kuamua kuisaidia hadhira kuelewa maana inayokusudiwa kwa kutumia vitendo, ishara na vitu mbalimbali.

Bibi Kassam huwapa wanafunzi wake muda wa kuandaa na kukariri hadithi zao. Wanapokuwa wanafanya kazi hii husimamia maendeleo yao na wakati mwingine huweza kufupisha ama kurefusha muda wa maandalizi. Alibaini kuwa wanafunzi wanapendelea kuandaa na kuigizia kazi zao nje.

Kwa wanafunzi 80, itachukua muda mrefu kama makundi yote yataigiza darasani. Katika siku ya kuigiza hadithi, Bibi Kassan huwaagiza wanafunzi waunde maduara manne ambapo kila duara linakuwa na makundi manne. Huyapa namba makundi katika kila duara kuanzia 1-4. Kikundi cha 1 huigiza katikati ya duara kwa ajili ya kikundi cha 2,3 na 4, kisha kikundi cha 2 huigiza kwa ajili ya kikundi cha 1,3,na 4 na kuendelea hadi makundi yote yamalize mzunguko

Baada ya uigizaji, Bibi Kassam, hukitaka kila kikundi kujadili juu ya kile walichojifunza. Hufikiri juu ya kile ambacho mwanafunzi mkimya darasani mwake alichoonesha kuhusu uelewa wake wa siku ile na namna anavyoweza kutumia taarifa hizi kuandaa hatua nyingine ya kujifunzia.

Nyenzo-rejea muhimu: Kufanyakazi na madarasa makubwa na/au madarasa ya viwango mbalimbali inatoa mawazo ya ziada kwa ajili ya kufundishia madarasa makubwa.

Shughuli muhimu: Kuigiza hadithi kwa ajili ya hadhira

Waagize wanafunzi kujigawa katika vikundi vya watu sita sita. Waagize wanafunzi ::

Kukumbuka kuhusu hadithi walizosimulia na kusikiliza

Kuamua ni hadithi ipi wanadhani itakuwa bora kuigizwa kwa ajili ya darasa ambapo kila mmoja ataweza kuelewa na kuifurahia. Kikundi zaidi ya kimoja kinaweza kuchagua hadithi ileile.

Wateue wahusika wote na kuamua kila nafasi itachukuliwa na nani. Watahitaji pia kuwa na msimuliaji.

Toa maamuzi juu ya lugha (z)itakayotumika, athari za sauti, matumizi ya ishara,mavazi, na vitu vitakavyosaidia kuipa hadithi uhai na nani ataleta Nyenzo-rejea zipi.

Wape muda wa kukariri na kuweka muda maalum kwa ajili ya uigizaji. Simamia kila kikundi na kuwasaidia kadiri inavyowezekana kwa kutoa mawazo na mapendekezo juu ya njia ya kufanya kazia.

Itake hadhira kutoa kuleta mwitikio kwa kila kikundi. ( Tazama Nyenzo-rejea 2: Tathmini uigizaji wa hadithi katika vikundi ).

Kama utaweza, rekodi hadithi zitakazoigizwa.Vinginevyo chukua dondoo kwa ajili ya matumizi ya baadaye.

Hadithi zinaweza kuigizwa mbele ya wazazi na viongozi wa jumuia katika eneo lako kwa lengo la kukusanya michango kwa ajili ya kununulia nyenzo za darasa lako.

Nyenzo-rejeaya1: Mfano wa barua ya mwaliko